Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Wizara hii kupigania ongezeko la bajeti, pia irekebishe sura yake ya bajeti. Haya ni maoni yangu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Bajeti yetu bado ni ndogo sana, shilingi trilioni 1.4; ni vema tufuate azimio la Abuja (E.F.A Goals). Bajeti ya Elimu ifike ifike 6% ya Tanzania GDP. Mfano, bajeti ya mwaka 2014, GDP ilikuwa inakadiriwa kuwa trilioni 100+, hivyo bajeti ya elimu ingekuwa shilingi trilioni 6.055.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Bajeti ya Elimu kwa matumizi ya kawaida, kujumuisha mikopo ya wanafunzi, nashauri siyo vema bajeti ya maendeleo kujumuisha mikopo ya wanafunzi; hii ina-mislead budget structure ya Wizara. Mbona ununuzi wa magari inawekwa kwenye matumizi ya kawaida?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Idara Ukaguzi wa Elimu itengewe bajeti ya kutosha na iongezewe rasilimali za kutosha ikiwemo rasilimali watu. Kwa sasa mawanda ya ukaguzi ni madogo, yaani asilimia 20 tu. Ni vema ukaguzi uweze kufikia angalau asilimia 30, itasaidia kugundua mapungufu na kufanya marekebisho mapema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Wizara hii ifanyie kazi tafiti zilizofanyika pamoja na ripoti za CAG hususan maeneo ya value for money, audit (VFM Audit). Mfano, wanafunzi kutofanya vizuri masomo ya hisabati, viwango vya ufaulu kwa watoto wa kike na kadhalika, Wizara ifuatilie maoni hayo ili tufanye vizuri na kuinua viwango vya elimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Waziri atusaidie kuanzisha Shule za High School katika Jimbo la Ushetu hususan Shule za Bulungwa Secondary School (Kata ya Bulungwa) na Mweli Secondary School (Kata ya Ushetu). Mimi Mbunge na wananchi tutahamasishana kuongeza madarasa na mabweni, naomba Wizara mtuunge mkono. Naomba kuwasilisha na naunga mkono hoja.