Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Spika, naanza kwa kuunga mkono hoja.

Mheshimiwa Waziri Mkuu Jimbo la Nkasi Kusini lina Tarafa moja ya Wampembe yenye kata nne, mawasiliano ya barabara ni magumu yaani hakuna kabisa barabara, kwa hiyo kuna shule za msingi zipatazo kumi shule hizi zina hali mbaya na hazitembelewi na wataalam wa ubora wa elimu hawafiki huko zaidi nafika Mbunge na wakati mwingine Mheshimiwa DC.

Kwa hiyo, shule hazijatembelewa miaka yote mitano ni Mbunge nimekuwa nikiwatembelea, ofisi za walimu ni chini ya mti. Shule hizo ni Lupata, Mkiringa, Mlalambo, Lusembwa, Itanga, Tundu, Lolesha na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, hoja ya pili; bajeti ya mwaka jana ilionesha kuna mipango ya kununua meli mpya katika Ziwa Tanganyika na kuwa meli ya Liemba itakarabatiwa, lakini katika bajeti hii haijanipa matumaini na tulishawaambia wananchi. Leo hakuna fedha wala mwendelezo wa mipango iliyosemwa katika bajeti iliyopita.

Mheshimiwa Spika, wavuvi wa Ziwa Tanganyika wanasumbuliwa sana na zaidi wanachanganywa na wataalam wa Wizara husika wanaambiwa nunuweni nyavu size fulani wakinunua kwa maelekezo yao wanasema nyavu hazifai na zinachomwa, wananchi wanapata hasara. Tuelezeni kwa nini mnafanya hivyo. Mheshimiwa Waziri Mkuu lione jimbo hili.