Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Martin Alexander Mtonda Msuha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. MARTIN M. MSUHA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote na mimi nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano, Mheshimiwa John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri anayoendelea kuifanya ya kutuletea maendeleo. Tumeona kwa macho miradi mikubwa inayotekelezwa. Lakini pia nichukue nafasi hii kukupongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa utendaji wako uliotukuka na kwa hotuba nzuri ya bajeti ya ofisi yako. Baada ya pongezi hizo sasa nianze kuchangia kama ifuatavyo:

Mheshimiwa Spika, nianze na suala la afya. Napenda kuchukua fursa hii kuishukuru Serikali kwa kutuletea fedha kiasi cha shilingi milioni 400 kwa ajili ya upanuzi wa Kituo cha Afya Mapera. Wananchi wa Tarafa ya Hagati wamenituma salamu zao za pongezi kwa Serikali ya awamu ya tano.

Hata hivyo tunaomba walau tungepata tena shilingi milioni 500 kwa ajili ya upanuzi wa Kituo cha Afya cha Kata ya Matiri ambayo ina wakazi wengi. Ombi letu lingine ni kuhusu gari ya dharura ya wagonjwa kwa maana ya ambulance. Ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, kuhusu TARURA, tumeshuhudia mvua nyingi sana katika msimu huu. Mvua hizi zimeharibu miundombinu ya barabara kwa kiwango kikubwa sana. Ushauri wangu ni kuwa Serikali ifanye upembuzi wa kina kila Wilaya ili kubani ukubwa wa tatizo. Baada ya zoezi hilo katika bajeti hii litengwe fungu maalumu kwa ajili ya kurekebisha miundombinu iliyoharibiwa na mvua hizo.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu wa pili katika eneo hili ni kuwa bajeti ya TARURA ipande kufikia walau asilimia 70.

Kuhusu Mfuko wa Wanawake, Vijana na Walemavu, ushauri wangu katika eneo hili ni kwamba Serikali ione umuhimu wa kuweka ukomo wa kipindi cha kuchangia inside indefinitely. Kwani zipo Halmashauri zenye makusanyo makubwa sana ya ndani. Hivyo kama michango hiyo haitawekewa ukomo wa miaka ya kuchangia basi fedha hizo zitakuwa ni nyingi na pengine kupelekea matumizi mabaya.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha na naunga mkono hoja.