Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Spika, kwanza nikushukuru wa kunipa nafasi lakini nianze kwa kumshukuru Mwenyenzi Mungu Allah Subhanahu Wataala kwa kutujalia afya njema na kuweza tena kupata fursa ya kuchangia katika bajeti ya mwisho kabisa katika kupindi hiki cha kwanza cha kukitumikia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, nianze kwa kuunga mkono hoja na nina tambua kazi nzuri zinazofanywa na Ofisi ya Waziri Mkuu akishirikiana vizuri na Mawaziri wake Mheshimiwa Jenista, Mheshimiwa Angela, Wasaidizi wake Mheshimiwa Mavunde na Mheshimiwa Ikupa mmefanya kazi kubwa sana.

Mheshimiwa Spika, lakini pamoja na haya mimi leo nina jambo moja tu, na jambo hili ninalielekeza kwa msajiri wa vyama vya siasa. Mheshimiwa Spika mwaka jana tuliboresha sheria ya vyama vya siasa na kuumpa nguvu sana msajiri wa vyama vya siasa ili awe meno katika kuvisimamia vyama vya siasa hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, sasa nataka nijue ni lini msajiri wa vyama vya siasa atakuwa amejiridhisha kwamba matukio ya fujo siasa za chuki kuamsha mihemuko ya hasira kwa wananchi zinazofanywa na Chama cha Demokrasia na Mandeleo CHADEMA kuwa ni sababu za tosha ya kukifuta chama hiki.

WABUNGE FULANI: Aaah tulia wewe!

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Spika, chama hiki kimesababisha fujo nyingi na moja kati ya fujo iliyofanyika tarehe 16 Februari, 2018 iliyopelekea kifo mdogo cha Akwilina Akwiline Bafutah. Hapa nina hukumu ya Kesi ya Jinai Namba 112 kesi ya mwaka 2018 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Spika, kwa faida ya Bunge lako naomba kunukuu Shauri Na. 4 katika kesi hiyo, kesi hiyo ilikuwa na mashauri 13. Na. 4 inasema hivi:-

“Particularly of the force account are that on 16th February, 2019 along Kawawa Road at Kinondoni Mkwajuni area within Kinondoni district in Dar es Salaam Region jointly and together with more than twelve other persons not in quote having riotously assembled in disobedor of proclamation to dispense made SP Gerald Thomas Nginja failed to dispence...”

SPIKA: Labda jambo moja Mheshimiwa shauri hilo limekatiwa rufaa au halijakatiwa rufaa?

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Spika, halijakatiwa rufaa.

SPIKA: Nawauliza upande huu.

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Spika, notes ya rufaa imeshatolewa na rufaa imeshakatwa kwa hiyo namshangaa anavyohaika tena…

SPIKA: Basi liruke tu…

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Spika, endelea tu halafu utafisiri kwa Kiswahili baada ya hicho kingereza.

SPIKA: Kwa ajili ya taarifa hii ambayo tumeipata. Endelea ana hoja yako.

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Spika, naendelea na hoja yangu kwa maana niache kunukuu kwa sababu wametoa notes ya rufaa na rufaa haijashikiliwa na kwa sasa hukumu halali ya public ni public document inaweza kutumika mpaka mahakama nyingine itakavyosema vinginevyo ndio maana nimeichukua hapa kuinukuu.

WABUNGE FULANI: Endelea endelea!

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Spika, katika shauri hili Na. 4 fujo zao za kukataa amri halali ya polisi zikasabisha kifo cha huyu binti Akwilina Akwilini Bafutaa. Lakini kibaya zaidi chama hiki hakionyeshi kujutia tukio hili, hukumu hii ilivyotoka chama hiki tulitegemea kama viongozi wa wananchi wangetoka kwenda kuiomba samahani na kuipa pole familia ya huyu binti marehemu. Lakini wao wakaanza kufanya vikao na waandishi wa habari vya kisiasa vya kujijenga kisiasa wakafanya vikao asubuhi mchana na jioni wakawa wanawaita waandishi wa habari wakilia kwa furaha ya shauri hili kuisha. wakati hawa wanalia kwa furaha mama wa marehemu Akwilina analia kwa uchungu. Wakati hawa wanafuata machozi ya furaha mama yake marehemu Akwilina hana mtu wa kumfuta chozi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama sio sisi wakumesemea mama Akwilina ambaye amempoteza mtoto kwa fujo za CHADEMA ni nani mwingine anaweza kumsemea? Kwa hiyo, majigambo waliyokuwa wakifanya mbwembwe za kuchangishana fedha walizokuwa wazikifanya hazikuwa zinafanywa dhidi ya CCM, hazikuwa zinafanya dhidi ya Serikali zilikuwa zinafanya dhidi ya mama yake Akwilina aliyepoteza mtoto. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mambo haya kama msajiri wa vyama vya siasa anaendelea tu kuyaangalia tunakwenda wapi? Na mimi nikukumbushe hizi hatua za kuachana na ubinadamu wanapiga kila siku, walianza kila ikitokea msiba labda wa CHADEMA aaah! Labda au wa Mbunge wa chadema au mwana CHADEMA mwenzao wakawa wanageuza misiba hiyo sio kuwa sehemu ya mbaombolezo bali kuwa jukwaa la kisiasa.

Mheshimiwa Spika, nikukumbushe wakati wa msiba wa marehemu Kasuku Bilago, wewe na ofisi yako mlikuwa mkishirikiana vizuri na familia ya marehemu Bilago. Ukafunga safari hapa mpaka Kankongo kwenda kuzika kwa tarehe ambayo umepanga. Kufika kule CHADEMA wakaairisha ule msiba usizikwe siku ile ili wewe usizike wao waweze kufanya siasa siku inayofuata. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tukiendelea kuyavumilia haya tunatengeneza siasaya aina gani? Ifike mahala msajiri awe mkali asilichoshe jeshi la polisi kufanya vitu ambavyo na yeye pia ana nafasi ya kuweza kuvifanya. Maadili ya vyama vya siasa yanasimamiwa na msajili iwa vyama vya siasa yanasimimiwa na msajiri wa vyama vya siasa. Hapa katika haya mauaji ya marehemu Akwilina wenyewe walipanga wafe watu 200, ukisoma shauri Na. 10 ambalo ameshtakiwa Mheshimiwa Mbowe peke yake katika kesi hiyo hiyo, muendesha mashtaka ana mnukuu wakati anawaanda sasa ili watoke wakati wanaingia mtaani kwamba wafe angalau watu 200.

Mheshimiwa Spika, ule ulikuwa ni uchanguzi mdogo wa jimbo moja Kinondoni akafa mtu mmoja katika target yao ya watu 200. Tunaelekea uchaguzi mkuu kila kata kutakuwa na uchaguzi kila jimbo litkauwa na uchanguzi nchi nzima itakuwa na uchanguzi hivi unajua wamepanga kuua watu wangapi? Lakini wewe mwenyewe ni shaihidi baadhi ya Wabunge hapa mara kadhaa wanasimama wanasema mimi nisingetangwa kama watu wawili wasingekufa mimi singetangazwa kama watu watatu wasingekatwa miguu. Haya yote ni mwendelezo wanayoyapanga wenzetu, sisi tunapanga kwenda kushinda majimbo wao wanapanga kwenda kuua watu msajili wa vyama vya siasa yupo wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, haya mambo ni lazima kama Bunge tuamue, tuamue kwamba tunalaani siasa hizi zinazofanywa na CHADEMA. Hata kama msajili atachelewa, lakini sisi kama Bunge part yetu tuifanye. Nilikuwa hata ninapata hisia kwamba mwishoni wa mchango huu nitoe hoja angalau tukatoe pole kwa familia ya Akwilina kwa kilichotokea tukamfute chozi huyu mama haiwezekani anaonewa mtu mmoja anashambuliwa na taasisi fulani tena ya viongozi wengine ni Wabunge halafu tukaa kimya tu ni lazima huyu mtu afutwe chozi. Na wakumfuta chozi sio hawa waliosababisha mauaji ya mwanae ni sisi tunayeyaona haya kwa mbali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tukiyaacha haya mambo na msajili akaendelea hivi hivitutaipeleka hii nchi kubaya. Naunga mkono hoja. (Makofi)