Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii adimu ili niweze kuchangia bajeti kuu ya Serikali. Kwa sababu ni mara yangu ya kwanza kama Waziri wa Viwanda na Biashara naomba uniongezee dakika moja ya kushukuru. Nianze kwa kumshukuru Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuendelea kuamini vijana kwamba tunaweza kuweka mchango mkubwa katika Taifa hili. Mheshimiwa Rais Mwenyezi Mungu akubariki sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia nimshukuru Makamu wa Rais, Waziri Mkuu pamoja na wewe, pamoja na Bunge kwa support ambayo mnaendelea kunipa katika kutumika wananchi na kutumia Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nianze kwa kushukuru sana kwa michango ambayo Waheshimiwa Wabunge wametoa katika kuchangia hii bajeti kuu ya Serikali. Michango mikubwa ambayo inahusu Wizara yangu imejikita zaidi kwenye masoko ya uhakika kwa mazao ya wakulima wetu na nitatumia muda mwingi kuzungumzia hili kwa sababu ya umuhimu wake. Mheshimiwa Rais wetu amekuwa akizungumzia nia ya kuunganisha kilimo na viwanda kwa sababu tukifanya hivyo tutawainua wakulima wengi nchini kwenda kwenye uchumi wa kati, kwa hiyo hoja yangu imejikita zaidi kwenye industrialization agriculture.

Mheshimiwa Spika, nikianza na mazao ya kimkakati, hata leo imetolewa mwongozo kuhusu zao la pamba. Pamoja na jitihada nzuri za Serikali kusaidia Ginners nchini, lakini wakulima wetu wamehamasika kwenye upande wa zao la pamba, uzalishaji umetoka tani 222,000, msimu huu tunategemea kuvuna tani zisizopungua 400,000.

Kwa hiyo kuendelea kutegemea Ginners peke yao kama soko la wakulima wa pamba hatutaweza kutoka kwenye mkwamo wa bei kushindwa kupanda. Kwa hiyo katika hili Serikali tumeazimia kuhakikisha textiles ambazo zilibinafsishwa lakini hazifanyi kazi, baada ya Bunge hili naanza nao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Textiles nchini zilikuwa 32, sasa hivi zimebakia tano ambazo zinafanya kazi, wengi wamekiuka mikataba ile ambayo walisaini kwa mujibu wa ubinafsishaji. Sasa Serikali tunataka kuhakikisha textiles hizi zinafanya kazi ili wakulima wa pamba wanapolima, tusitegemee tu kwamba Ginners liwe soko peke yake. Ile sera ya C to C (Cotton to Cloth) sasa tunaanza kwenda kwa vitendo kuhakikisha mkulima anapovuna shamba, soko lingine linaenda kwa Ginners lakini soko lingine linaenda kwenye textiles ili ziweze kutengeneza garments, ziweze kutengeneza pamba nyuzi na wakulima wetu wapate soko la uhakika.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hili, nitumie nafasi hii kutoa clarification kuhusu zao la korosho. Kumekuwa kuna upotoshaji mkubwa sana na upotoshaji huu umepelekea dunia kuamini kwamba korosho yetu imeoza kumbe siyo kweli. Baada ya kuapishwa nimetumia wiki nzima nikienda ghala kwa ghala kwenye mikoa inayolima korosho, korosho yetu iko katika hali nzuri.

Kwa hiyo Waheshimiwa Wabunge niwaombe tuweke utaifa mbele na uzalendo mbele, hakuna korosho ambayo iko reject hata moja, korosho yote ni grade I na grade II. Sasa tunapowasiliana na wanunuzi duniani kuna watu bado wanaendelea kupotosha kwamba msinunue korosho ya Tanzania siyo safi.

Mheshimiwa Spika, nitumie Bunge hili kuwaambia wananchi, Serikali is open for business, korosho yetu ina ubora, Waheshimiwa Wabunge wanaotoka kule wanajua. Tuwe wamoja, tushirikiane Taifa moja kuhakikisha tunawasaidia wakulima wa korosho, tutoe hii korosho lakini msimu unaokuja tukijipanga vizuri hata zao la korosho bado lina potential kubwa ya kuwasaidia wakulima wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kwa sababu ya muda niseme kwamba kuhakikisha viwanda vilivyobinafsishwa vinaanza kufanya kazi, lakini pia tunafungua fursa za masoko za kimataifa kwa kushiriki katika forum za kimataifa kama World Economic Forum, kuhakikisha tunashirikiana na Balozi zetu, kuwa na mkakati mzuri wa kutafuta masoko ya uhakika. TANTRADE tunai-reform upya ili iweze kujikita katika kuhakikisha inakuwa interface ya nchi na dunia kutafuta masoko ya wakulima wetu.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo, Mheshimiwa Mpina, Waziri wa Mifugo na Uvuvi pamoja na Mheshimiwa Japhet Asunga, Waziri wa Kilimo tumejipanga katika kuhakikisha tumejipanga katika kuhakikisha tunafungamanisha hizi sekta na kuhakikisha tunaongoza Serikali na Watanzania kwenda kwenye uchumi wa viwanda kupitia value adding. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, kwa sababu ya muda kutotosha nimalizie na suala la blueprint.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Mbilinyi.

T A A R I F A

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, nataka nimpe taarifa Mheshimiwa Waziri mpya wa Viwanda na Biashara anayechangia kwamba hivyo viwanda vilivyobinafsishwa anavyozungumzia kwamba baada ya Bunge atarudi kuanza navyo ili avirudishe kazini, nataka nimpe taarifa kwamba vingi hata ile mitambo hakuna ilishang’olewa. Kwa hiyo anaona kiwanda ni kama godown tu lakini ndani mitambo hakuna tena, kwa hiyo kama kilikuwa kiwanda cha textile ndani ya hicho kiwanda hatakuta mitambo kwenye maeneo mengi sana. Naomba alijue hilo.

SPIKA: Mheshimiwa Waziri, endelea.

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, taarifa ya ndugu yangu Mheshimiwa Sugu siipokei kwa sababu sisi viwanda vilivyobinafsishwa hata infrastructure bado ni value na tunataka tukae na wawekezaji wale ambao wako serious tukae nao tuingie joint venture, waingie kwenye mpango kazi wa kusaidia kuhakikisha tunachakata mazao ya wakulima kwa ajili ya soko la ndani. Tanzania ni member wa East Africa tunalipa fees kila mwaka kushiriki katika hiyo membership, ni member wa SADC, hayo yote ni masoko ambayo tungependa nchi yetu iwe ni production hub kwa ajili ya hayo masoko pamoja na maeneo mengine ya dunia. Kwa hiyo, katika hili niwape tu confidence kwamba Serikali tukihakikisha vile viwanda vilivyobinafsishwa vinafanya kazi wakulima wetu hawawezi kupata shida katika masoko ya mazao yao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilitaka kumalizia na suala la blueprint, Serikali tumeanza katika bajeti hii kodi kero 54 zimeondolewa na tayari tuna action plan. Kwa hiyo ni kukuomba wewe pamoja na Wabunge tushirikiane katika kuhakikisha tunaondoa unnecessary red tapes ambazo zimekuwa zikiwakumba wafanyabiashara nchini. Serikali katika hili nia yetu na tumejipanga vizuri katika kuhakikisha tunafanikisha katika hilo. Kikubwa ni change of mindset yaani Watanzania tuichukulie biashara kama ni fursa ya kutengeneza ajira kwa vijana na akina mama nchini lakini Private Sector Development ndiyo injini ya kusaidia uchumi wetu ukue katika namna ambayo ni sustainable.

Kwa hiyo Watanzania ile mindset ya ku-frustrate biashara tutoke huko tu-facilitate kila mmoja katika nafasi yetu ili private sector iweze kukua na kutengeneza ajira kwa vijana na akinamama. Tutafanikiwa katika hili kama tutashirikiana kuhakikisha blueprint na action plan yake wote tunashirikiana kwa pamoja kuhakikisha inatekelezwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Wizara yangu tutahakikisha sera za viwanda ambazo ni za mwaka 2003 nilizozikuta, tunafumua zote na ku-update kwa sababu ukitegemea kwenda kwenye uchumi wa viwanda kwa kuwa na injini ya Vits inayovuta Semi-trailer hatuwezi kufika. Kwa hiyo pa kuanzia ni kuhakikisha sera hizi za zamani za 2003 tunazi-overhaul ili ziweze ku-reflect priority ya nchi ya kwenda kwenye uchumi wa viwanda.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii. (Makofi)