Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. OMARY M. KIGUA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kwamba nimechangia hotuba kwa kuzungumza naomba tena kusisitiza juu ya hoja yangu ya kuongoza Tax base ambayo inaweza kuongezeka kwa kuzingatia vifungu vipya kwenye jedwali Na.2 ukurasa 42 wa hotuba ya Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2014 idadi ya Watanzania ni 55,890,744 kwa tofauti ya umri kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2014 Idadi ya Watanzania ni 55, 890,747 kwa tofauti ya umri:-

(1) Umri kati ya mika 0 – 5 watu 9,628,845;

(2) Umri kati ya 6 – 19 watu 20,836,171;

(3) Umri kati ya 20 – 64 watu 23, 691, 680;

(4) Umri kati ya 65 na kuendelea watu 1,734,051

Mheshimiwa Naibu Spika, nitajikita kwenye kundi namba (3), umri wa mika 20-64 ambapo ndipo kwenye idadi kubwa. Hapa ukichukua Idadi ya watu 3,000,000 tu, tukizingatia kuwa hawa si miongoni mwa wale wadogo kwenye kundi la sekta isiyo rasmi, na ni kundi jipya. Wakifanikiwa kutoa shilingi laki moja (100,000) Serikali itaweza kukusanya bilioni mia tatu. Makundi mengine yaliyobaki yanaweza kusaidia Serikali kupata takribani billion mia saba; hii itakuwa imesaidia Serikali kupata takribani trillion moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, Watanzania ambao hawajalipa wako wengi. Serikali inakusanya kodi kwa watu wale wale na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) hawajafanya jitihada za kutosha kuongeza wigo wa idadi ya watu kulipa kodi. Nashauri; umefika wakati wa kupunguza mzigo wa Watanzania wanaolipa kodi kuwa ni wale wale.

Mheshimiwa Naibu Spika, kila siku kila Mtanzania anatumia barabara, zahanati viwanja vya ndege, shule na vyuo vikuu bila kulipa kodi; ni lazima sasa kila Mtanzania alipe kodi kwa hiyari, na hili linawezekana.

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo lingine ambalo ningependa kutoa ushauri ni eneo la wataalamu wa TRA wanaofanya makadirio (tax Assessors).Eneo hili ndilo ambalo limelalamikiwa sana na Watanzania hususani wafanyabiashara. Hapa lazima wawepo watumishi wenye weledi mkubwa wa tasnia au elimu ya kodi; watu ambao watakuwa na uadilifu wa hali ya juu pamoja na uzoefu katika sekta ya kodi kiwe ni kigezo kikubwa. Si busara kijana awe amemaliza Chuo Kikuu na ana muda mfupi kazini halafu anapewa jukumu la ukadiriaji wa kodi

Mheshimiwa Naibu Spika, Naunga mkolo hoja.