Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Eng. Christopher Kajoro Chizza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. ENG. CHRISTOPHER K. CHIZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nawapongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watndaji kwa kuleta mapendekezo ya mapato na matumizi mazuri. Baada ya kuchangia kwa mazungumzo sasa napenda kuchangia maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Kuhusu Haja ya Kuweka Mkakati Maalum wa Kuendeleza Kilimo cha Umwagiliaji. Bado nchi yetu ni ya wakulima, kilimo kitaendelea kuwa muhimili wa kuimarisha utoshelevu na usalama wa chakula, kuchangia Pato la Taifa na pia kilimo kitaendelea kuwa chanzo cha malighafi ya viwanda ambavyo tunavijenga sasa. Ili tufikie malengo hayo, ni lazima tukubali kufanya uamuzi wa maksudi wa kuwekeza katika kilimo. Tanzania ilikubaliana na nchi wanachama wa SADC kupitia Azimio la Maputo kwamba kila nchi mwanachama itenge asilimia 10 ya bajeti yake kwenye sekta ya kilimo ili kuharakisha ukuaji wa sekta hiyo. Je, utekelezaji umefikia wapi.

Mheshimiwa Naibu Spika, takwimu zifuatazo zinaonesha haja ya kuwekeza katika kilimo.

(1) Eneo linalofaa kwa kilimo ni 44,000,000 Ha

(2) Eneo linalolimwa ni 14,000,000 Ha

(3) Eneo linalofaa kwa umwagiliaji 29,400,000 Ha

3.1. High Irrigation Dev. Potential 2, 300,000 Ha

3.2. Medium Irrig. Dev. Potential 4,800,000 Ha

3.3. Low Irrig. Dev. Potential 22,300,000 Ha

3.4. Eneo linalomwagiliwa (2019) 47,052 Ha. Only

(4) Zana za kilimo

4.1. Wakulima wanaotumia zana (matrekta)-10%

4.2. Wakulima waotumia (zana) wanyamakazi 20%

4.3. Wakulima wanaotumia jembe la mkono 70%

Mheshimiwa Naibu Spika, takwimu hizo hapo juu zinadhihirisha maomba yafuatayo:-

(1) Ni lazima tuwekeze kwenye ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji (irrigation and drainage) ili tulitumie eneo linalofaa kwa umwagiliaji ambalo kwa sasa tumeliendeleza kwa takribani 0.1%.

(2) Tunahitaji kutumia zana za kilimo ili tuweze kulima eneo lote linalofaa kwa kilimo ambalo hivi sasa tumeliendeleza kwa takribani 33% tu (angalia pia taarifa ya CAG ya March 2019 Chapter 2, p.5 sec.2.1). Hatuwezi kuendekeza hekta milioni 44 kwa jembe la mkono. Nashauri Serikali ianzishe tractor hire and service centers ambazo zitatoa huduma kwa wakulima wadogo kwa sababu haitawezekana kila mkulima kujinunulia zana za kilimo.

(3) Cropping intensity and productivity, kwa kuwekeza katika kiundombinu na mashamba ya umwagiliaji tutaweza kuongeza uzalishaji kwa kulima eneo moja zaidi ya mara moja kwa mwaka (increased cropping intensity) kwa kuwa maji yatakuwepo kwa kuwa maji yatakuwepo. Aidha ni rahisi kuongeza uzalishaji wa mazao katika eneo moja kwa kuwezesha upatikanaji wa maji na pembejeo na huduma za ugani (increased productivity/ production per unit area).

Mheshimiwa Naibu Spika, Masoko ya Mazao.

(1) Tunapokuwa na ziada ya mazao, hususan nafaka, nashauri Serikali iweke utaratibu (kama inavyofanya kwenye sukari) wa kuwasimamia wafanyabiashara ili wauze ziada nje ya nchi.

(2) Serikali ianzishe mfuko wa kuhimili bei za mazao (Price Stabilization Fund) pindi bei za mazao zinapoanguka hasa katika soko la dunia. Mwaka 2013, Serikali, kupitia Wizara ya Kilimo ilianzisha mchakato wa price stabilization fund kwa mazao manne ya Korosho, Kahawa, Pamba na Tumbaku. Kwanini mchakato huo haukuendelea? Mimi nashauri wazo hilo lifanyiwe kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.