Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. SUZANA C. MGONUKULIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ukusanyaji duni wa mapato unavyoathiri utekelezaji wa bajeti ya Serikali unatokana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imeonesha udhaifu na uwezo mdogo wa ukusanyaji mapato.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ilitakiwa kukusanya shilingi trilioni 17.315 badala yake, ilikusanya shilingi trilioni 15.386 ikiwa ni pungufu ya shilingi trilioni 1.929.

Mheshimiwa Naibu Spika, natolea mfano wa ukusanyaji wa kodi za majengo, nikuombe Waziri jaribu kuandaa mfumo wa kushirikisha Serikali za Mitaa yaani maafisa wa TRA wawatumie watendaji wa mitaa kwa kuwa wlae watendaji wa mitaa kazi zao za kila siku wako mitaani nyumba kwa nyumba, zoezi hili litaleta mafanikio makubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na mfumo wa kodi umekuwa ukilalamikiwa sana kwa miaka mingi na jamii ya wafanyabiashara ambao ndio walipa kodi si shirikishi wala si rafiki, jambo ambalo limesababisha kukwepa kodi na hivyo kupunguza wigo wa walipa na mapato ya Serikali, nikuombe Waziri wa Fedha maeneo ya muhimu unda Kamati Maalum ziangalie kama tatizo hili bado linakuwa ili litafutiwe uvumbuzi.