Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuendelea kutoa chanzo cha mapato ambacho kitasaidia kukuza mapato ya Serikali na kuondokana na utegemezi wa kodi ambazo hazina uhalisia mfano wa kodi za nywele bandia.

Mheshimiwa Naibu Spika, sote tunajua kuwa Sekta ya Utalii ni moja ya Sekta zinazochangia kwenye Pato la Taifa lakini ukweli ni kwamba hatujatumia rasilimali za utalii tulizonazo na kuwekeza ili tupate mapato ambayo kwa kweli yangesaidia kupunguza kodi kwenye maeneo mengine kama taulo za kie, nywele bandia, punguzo la PAYE kwa wafanyakazi, vitambulisho vya wafanyabiashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye mchango wangu wa kuongea nilieleza kidogo kwenye uwekezaji wa utalii wa fukwe (beach tourism), utalii wa meli (cruising tourism) na utalii wa mikutano, matukio (Mice tourism). Haya mambo hatujayaona na kuwekeza ili kuweza kukuza uchumi wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna fukwe nyingi sana za bahari kuanzia Mtwara, Dar es Salaam, Tanga, fukwe za ziwa, fukwe za visiwa. Tunahitaji kufanya classification za fukwe zetu ili tujue fukwe zenye mchanga, miamba na kdahalika, lakini pia tunaweza kutengeneza artificial beaches kwenye maeneo ambayo bado hayajatumika (beach resort). Mfano kule Bagamoyo (SES). Pale tukijenga beach resort yenye facility zote. Kule Kigamboni tunaweza kujenga connection center zenye hadhi za Kimataifa kwa Tanzania hatuna kwakweli zaidi ya ile AICC iliyojengwa na Mwalimu Nyerere. Tunahitaji Mataifa mbalimbali waweze kuvutika kuja Tanzania maana tuna uwanja wa ndege wa kisasa, tuna ndege, tujenge connection center kama za Barcelona, Rwanda na kwingineko. Tuwe na modern pitch ambazo zina accommodate michezo yote na ambazo wakati mwingine inageuka kuwa concert hall. Hapo kwa kweli tutaongeza idadi ya watalii.

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile ni wakati wa kuhakikisha convention center zetu ziwe hotel zenye sifa za kuweza kukalika/kupokea Marais wa nchi mbalimbali. Leo tuna Mkutano wa SADC lakini Jiji la Dar es Salaam sio tu halina uwezo wa kupokea ugeni huo lakini ukweli hoteli zenye sifa ya kufikia Marais ni hotel ya Hyatt tu ambayo hoteli hii ilikuwa ni ya Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia ni wakati sasa wa kuwekeza kwenye theme parks, najua wengi wetu tumesafiri nchi mbalimbali hata watendaji na tumeona ni jinsi gani hizi theme parks zilivyo. Tunaweza wekeza theme park katika Majiji kama Dar es Salaam pale pande game reserve ijengwe theme park, kule Mbeya pia pawe na theme park, Mwanza napo tuwe na theme park na Arusha. Hapa tunaweza kuongea na Disney ili waweze kuja kuwekeza kupitia PPP. Hakika hili likijengwa litasaidia kukuza uchumi na kuongeza mapato.

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile ili kuweza kurahisisha usafiri kipindi watalii wamekuja na kuweza kutembelea vivutio mbalimbali, hivyo ni vyema tufanye cruising terminal (cruise terminal). Mfano SGR na uwanja wa ndege terminal III vinahitaji kiunganishi cha Dar es Salaam, cruise terminal kama ile ya Kai Fan ya Hong Kong. Ijengwe pia Mtwara Cruise terminal, Tanga cruise terminal, hakika itasaidia mtalii anaenda Mtwara, Lindi kuona malikale under water experience, kule Mafia wakija Dar es Salaam wanashuka kirahisi na kuungana na SGR kuelekea Mikumi na kwingineko. Leo fukwe za Saadan ukilinganisha na Costa Rica, Mtwara na Seychelles, Dar es Salaam, Durban/Cape town. Walikuja hapa watalii walishindwa kutumia kamba, wengine ni wazee na ni aibu.