Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Martha Jachi Umbulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. MARTHA J. UMBULLA: Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa kukupongeza sana wewe na Naibu wako kwa kazi kubwa na nzuri. Baada ya pongezi nijikite kwenye maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Kilimo; hakuna Mtanzania mzalendo atakayeacha kuchangia sekta hii kwa ustawi wa Taifa letu na ustawi wa mtu mmoja mmoja. Umuhimu wa kilimo usipokuwa reflected na bajeti hii kutakuwa na tatizo kwa kuwa, ni sekta inayotegemewa na watu wengi na tegemeo kwa malighafi ya viwanda vyetu. Tunaambiwa sasa hivi Pato la Taifa limepandishwa na sekta ya madini na utalii, ombi langu kwa Serikali, tusibweteke na hali hii tuhakikishe sekta ya kilimo inaboreshwa. Kwa sasa uzalishaji unashuka. Serikali ifanye utafiti wa mazao ya wakulima wadogo, wa kati na wakubwa ili kutatua changamoto zao ambazo kwa kweli hazifanani.

Mheshimiwa Naibu Spika, ningeomba pia, kwa kuwa wakulima wetu hamasa kubwa ni soko la uhakika la mazao yao, naomba wakulima waruhusiwe kuuza mazao yao nje au popote wanapopata soko. Viwanda vyetu vikiimarika tutazuia uuzaji nje ya nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wangu wa Manyara hauhitaji hata mafunzo kwa wakulima kwa sababu kilimo ni sehemu ya maisha yao. Wakipata soko la mahindi, mbaazi, maharage, vitunguu, basi kilimo kitapanuliwa na kuboreshwa maradufu.

Mheshimiwa Naibu Spika, mifugo. Nikiri kabisa kuwa sekta hii ya mifugo haijapewa kipaumbele kinachostahili na wafugaji pia wapewe fursa ya kuuza mazao yatokanayo na mifugo. Nchi yetu imebarikiwa kuwa na mifugo mingi, lakini hatuna viwanda vya kusindika ngozi, hatuna soko la kuuza ngozi ndani ya nchi. Naiomba Serikali iruhusu uuzwaji wa ngozi ghafi nje ya nchi na pia ipunguze tozo mbalimbali zinazotozwa katika suala la uuzaji wa ngozi, hasa export levy iondolewe au ipunguzwe sana. Ufike wakati sasa Serikali nayo ione namna ya kuwaboreshea maisha wafugaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja.