Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, kuruhusu Baadhi ya Miji kufanya Biashara Saa 24; nafahamu ni suala la biashara kwa maana ya leseni inaeleza muda wa kufanya biashara, Hata hivyo, kama tunataka mapato (kupanua wigo) Wizara iongeze (take lead) kuhakikisha kuwa, baadhi ya miji kama vile Mikumi, Ruaha Mbuyuni, Ilulu, Mafinga, Makambako, Igawa na kadhalika iwe designated kama miji ya kibiashara saa 24 sambamba na miji mikubwa kama Dar-es-Salaam, Mwanza, Arusha, Mbeya na miji ya mipakani yote kufanya biashara saa 24.

Mheshimiwa Naibu Spika, Soko la DRC Congo hasa kwa Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini. Kuna soko kubwa la mazao Kongo Mashariki. Hata hivyo, ili kunufaika na soko hilo lazima upitishe bidhaa kwa njia mbili:-

(i) Tunduma – Kasulambesa – Lubumbashi

(ii) Dar-es-Salaam – Rusumo – Kigali – Bukavu mpaka Kigoma

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2018 wakulima wa Njombe walipoteza tani 600,000 za mahindi na mchele baada ya Zambia kuleta vikwazo maana na wao wanategemea Soko la DRC Mashariki. Hivyo, njia sahihi na isiyo na vikwazo ni kutumia Bandari ya Karema ambayo upande wa pili ni Momba au Kigoma – Kalamie na kuna soko kubwa mno, hivyo tukiimarisha bandari zetu tutaongeza tija na trade volume itaongezeka maradufu.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, yapo ya kufanyika kwa mfano kupitia JPC – Joint Permanent Commission ambayo haijafanyika since 2002. Kupitia JPC au mikutano ya ujirani mwema itafanikisha kuondolewa kwa vikwazo kadhaa. Kwa mfano, suala la visa ambayo ni dola 50 kwa dola 200, visa ya kibiashara, lakini pia SUMATRA kwa sheria na kanuni hairuhusu meli kubeba mizigo na abiria, lakini kwa DRC – Congo kutokana na hali yao meli za mizigo zinaruhusiwa na abiria, sasa wakivuka Lake Tanganyika wanapigwa faini dola 500, next week hawaji. Kwa mujibu wa World Bank, mwaka 2017 wafanyabiashara wadogo waliuza mchele DRC wa thamani ya dola 1.5m almost Tshs 3.5b. Hivyo, kuna fursa ya kuongeza trade volume kati ya Tanzania na DRC.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la Sukari; pamoja na mchango huu naambatanisha mawazo haya japo ni ya 2016. Kipo cha kujifunza, ili kuondokana na uhaba wa sukari hapa nchini.