Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja ya bajeti 2019/2020 na naipongeza Serikali katika utekelezaji wa Ilani ya CCM, 2015 kwa kiwango kinachoridhisha. Katika uboreshaji wa mazingira wezeshi kwa uendeshaji biashara na uwekezaji katika Wilaya ya Malinyi kuna fursa kubwa za uwezeshaji wa biashara ya kilimo cha mazao ya nafaka (mpunga, ufuta, mahindi) kupitia miradi ya SACGOT, FEED THE FUTURE, FOMAGATA (Miradi ya Kitaifa). Miradi hii ya kilimo cha biashara ili iweze kufanikisha ni muhimu kuwepo na uboreshaji wa miundombinu ya barabara kuu inayopita katika Ukanda huo wa SACGOT.

Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Mikumi – Ifaraka – Malinyi – Londo – Songea. Barabara hiyo ni muhimu sana kujengwa katika kiwango cha lami. Ujenzi wa barabara hii utatengeneza mazingira ya kushawishi na kuvutia wawekezaji kwa kuwa, eneo hilo linalopita katika Bonde la Mto Kilombero ambalo linafaa sana kama litatumika kikamilifu linaweza kutatua tatizo lote la upungufu wa chakula katika nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa muda mrefu imekuwa ikitoa ahadi ya ujenzi wa barabara hivyo, kiwango cha lami (Mikumi – Ifakara – Malawi – Londo – Songea), lakini ahadi hizo hazitekelezwi hivyo, kuathiri sana ushawishi na kuvutia wawekezaji wa kilimo cha biashara na viwanda katika maeneo ya Bonde la Kilombero kutokana na changamoto ya ubovu mkubwa wa barabara hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na naunga mkono hoja.