Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Kiteto Zawadi Koshuma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. KITETO Z. KOSHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kupata nafasi ya kuchangia hotuba ya bajeti kuu ya Serikali. Nianze kwa kusema kuwa, natambua zipo sekta mbalimbali zinazochangia katika ukuaji wa uchumi wa wananchi na pato la Taifa, zikiwemo sekta za madini, mawasiliano, fedha, kilimo na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, sekta ya kilimo ndiyo inachangia kwa asilimia kubwa na kutoa ajira kwa wananchi kwa wingi na hivyo kuondoa hali ya umaskini kwa wananchi. Hivyo basi, ni vyema Serikali ikawekeza kwenye kilimo kwa kutenga bajeti ya kutosha, bajeti ikiwa ni kubwa, mambo yafuatayo yataweza kutekelezwa:-

(a) Kufanya tafiti ya ardhi gani inafaa kwa zao lipi katika kila mkoa;

(b) Kufanya tafiti ya mbegu bora ili kuongeza uzalishaji ulio bora;

(c) Kuajiri Maafisa Ugani ili watoe elimu kwa wakulima ili walime mazao yenye viwango vya juu kwa ajili ya export na viwanda vya ndani; na

(d) Kuwekeza kwenye Taasisi ya Zana za Kilimo - CAMARTEC ili kukuza kilimo cha kisasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, tukiweza kuwekeza kwenye kilimo ndipo viwanda na sekta zingine zitakua.