Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuweza kuchangia machache kwa maandishi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia jambo moja ambalo sikuweza kulichangia kwa kuongea wakati wa mchango wangu kwa sababu ya muda.

Mheshimiwa Naibu Spika, uwanja wa ndege wa Morogoro. Nashukuru Serikali kwa kutupatia Meneja wa Kiwanja cha Ndege Morogoro Ms Esta Mwigune. Morogoro ni Mkoa ulio katikati mwa Jiji la Dar es Salaam pamoja na Jiji la Dodoma. Kwa sababu hiyo na sababu nyinginezo, Manispaa ya Morogoro inakua kwa haraka sana. Tunashukuru kwa Serikali kwa kuliona hilo na kuutambua Uwanja wa Ndege Morogoro.

Pili, Mkoa wa Morogoro tuna sehemu za utalii ikiwepo Mikumi, Selou pamoja na Udzungwa. Kwa kuutambua na kuujenga uwanja wa ndege wa Morogoro, kutaongeza kuja kwa watalii wengi, hivyo kuinua uchumi wa nchi yetu

Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo linalojitokeza sikuona fedha yeyote iliyotengwa ya kutengeneza/kujenga/ kukarabati uwanja wa ndege Morogoro, ingawaje tumeanza kupata wafanyakazi kama Meneja na wengineo. Ombi langu, naomba na kushauri uwanja huu wa ndege ukatengenezwe kwani ni wa manufaa kwa nchi yetu na hasa kufuatana na kukuza utalii.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kiwanja cha ndege cha Selou tulishaambiwa kuwa kitajengwa. Je, ni lini kiwanja hiki kitajengwa?

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana, nategemea nitajibiwa, baada ya hayo, naunga mkono hoja.