Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunapokuwa tunazungumzia maendeleo ya kiuchumi hatuwezi kuacha kuzungumzia suala zima la ubora wa watu, yapo matatizo mengi ambayo yamesababishwa kwa kiwango kikubwa siyo na sera au mfumo, lakini yamesababishwa pia na tatizo la ubora wa watu, kwa maana ya maarifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitoe mfano mdogo sana, ukiangalia Serikali inakusanya kwa mwezi bilioni 1,300. Katika kila bilioni 1,300 bilioni 580 inatumika kulipa wafanyakazi, kama sawasawa na kama asilimia 45. Sasa unaweza ukaona kwamba, asilimia 45 hii ni portion kubwa sana, lakini inaoneka ni kubwa kwa sababu ya uzalishaji ni mdogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo tunazungumzia uchumi wa viwanda. Kama Taifa tulishapiga hatua kubwa sana kwenye suala la uchumi wa viwanda toka miaka ya sabini, sabini na tano, cha ajabu tukapiga--reverse big time ukilinganisha uchumi wa viwanda wa sasa na uchumi wa viwanda wa miaka ya 1970 ni vitu viwili tofauti. Kwa mambo kama haya, hata ikitokea Baba wa Taifa Julius Kambarage Nyerere akafufuka leo, atakufa kwa stress ambazo zipo katika Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo tunazungumzia uchumi wa viwanda tunaambiwa vyerehani, tunaambiwa vyanzo vya mapato ni mawigi. Dunia kwenye Force Industrial Revolution, wanazungumzia artificial intelligence, asimame Waziri yeyote hapa aseme kama kwenye Wizara yake ameshafanya research akaangalia ni kwa kiwango gani artificial intelligence inakwenda kuathiri sekta yake au kwa kiwango gani inakwenda kunufaisha sekta yake, hakuna. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni vema tuka-invest bila kuogopa kwenye ubora wa watu. Ni mambo ya ajabu sana tunazungumzia uchumi wa viwanda na wakati hatu-invest vya kutosha upande wa watu. Ninaomba kipindi cha zamani tulikuwa tunaangalia kwenye soko la ajira tulikuwa tunapambana sana na Wakenya, lakini sasahivi tunakwenda kupambana na ma-robot kwa sababu, ya uwezo tulionao na nguvu tuliyotumia kuwekeza kwenye ubora wa watu wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa naangalia Google wamejenga center kubwa sana ya artificial intelligence pale Accra, Ghana, mwaka jana na wamealika nchi tisa kwenye timu hiyo kuhakikisha kwamba wanapata knowledge ya namna gani artificial intelligence inaenda kunufaisha katika Mataifa yao, kwa upande wa East Africa wamechukua Rwanda peke yake. Kwa hiyo, ni bora wakati tunafikiria uchumi wa viwanda, lakini tukawekeza kwa nguvu kubwa sana kwenye ubora wa watu wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nigusie pia suala la Deni la Taifa. Kwa muda mrefu sana tumekuwa tukipigia kelele suala la Deni la Taifa, mwaka 2016 nilileta maelezo binafsi humu ndani kuelezea ni kwa namna gani Deni la Taifa linakua kwa kasi kubwa sana, lakini mpaka leo Deni la Taifa limeendelea kuwa ni habari ambayo haina majibu ya kutosha. Badala ya kuendelea sasa kuangalia ukubwa wa Deni la Taifa ni muhimu sasa tukajielekeza kuangalia uhalali wa deni hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Waziri wa Fedha Dkt. Mpango atakapokuja hapa nimtake wakati anahitimisha kwa kutumia Audit Report ya Madeni kwa sababu najua Serikali mnakagua madeni, atuambie uhalali wa deni ambalo tunalilipa la bomba la gesi ambapo inaonekana kwa kiwango kikubwa deni hili limekuwa na kizungumkuti kikubwa. Tutaendelea kukamata wauza kahawa na wafanyabiashara wadogo kwa ajili ya kulipa madeni ambayo hayaeleweki watu waliingia katika utaratibu gani? Ninaomba Mheshimiwa Mpango afanye hivyo, atuambie gharama halisi ya gharama ambayo ilitumika kujenga bomba la gesi na atuambie tunalipa kiasi gani kila mwezi kufidia gharama hiyo ya bomba la gesi? Na kama hatafanya hivyo, nakusudia kuleta hoja binafsi Bunge lijalo, kutaka Serikali iunde Tume kwa ajili ya kuchunguza suala hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba pia, nigusie kwenye suala zima la TRA. Imekuwa ni kama utaratibu fulani hivi kwamba nchi nyingi ambazo ni za kimasikini zimekuwa na utaratibu wa kutengeneza muundo mkubwa sana wa Serikali na kuu-feed kwa gharama kubwa sana. Hii inaonesha ni kwa kiwango gani ambavyo tunakuwa tunakosa trust na private sector.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna Mataifa ambayo yameonesha trust kwa private sector kiwango cha kuzipa private sector mamlaka ya kutengeneza Mahakama. Kwa mfano kama Marekani, lakini sisi imefikia hatua kwa mfano TRA tunashindwa nini kutengeneza mfumo ambao utatusaidia kukusanya kodi kiurahisi?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano kupeleka ma- agency maeneo mbalimbali kama ambavyo mabenki yanafanya. Tunakuwa tuna ma-agency mbalimbali maeneo yote nchini ambayo inarahisisha zaidi ukusanyaji wa kodi. Ni vema tukawa tunakuwa innovative kuhakikisha kwamba, tunakusanya mapato na kuhakikisha kwamba tunafanya vizuri kwenye sekta ya uchumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. (Makofi)