Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Savelina Slivanus Mwijage

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. SAVELINA S. MWIJAGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia Wizara ya Elimu, kwa kuwa elimu ndio jambo la muhimu sana. Bila elimu hakuna Daktali, hakuna Pilot, hakuna Mwalimu hakuna Rais, hata viwanda ambavyo tunavisema ni bure, wala barabara, hakuna chochote! Sasa Serikali iwekeze kwenye elimu, tusifanye wimbo elimu bure, tuwekeze kwenye mashule. Bado wanafunzi wanakaa chini, hawana vyoo, hawana maji, hawana vitabu, hasa vitendea kazi vyote hawana. Watoto hawawezi kukaa chini; wataweza kuwa na akili?
Mheshimiwa Mwenyekiti, imekuwa tabia kwa Mwalimu, anakaa hadi anastaafu bila hata daraja la kwanza. Heshima ya Walimu iko wapi? Kazi kulalamikia malipo, kulipwa stahiki zao. Kuna wanaostahili toka mwaka 2014 na ni wengi zaidi, unategemea hao Walimu watakuwa na akili ya kufundisha. Serikali ilipe stahiki zao ili tujenge elimu bure.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye shule za binafsi tunaomba Wizara hii iangalie hata kama sheria nyingine ambayo itaweza kusaidia, tunasema watoto wapate elimu bure na karo zinakuwa juu. Hii watasoma watoto wa matajiri tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu madawati yaliyotajwa na Mheshimiwa Rais, nashauri, kwanini zisitolewe pesa kila Wilaya ya kutengenezewa huko huko kuliko kubebwa na kusambazwa? Je, hiyo gharama nyingine? Ni ushauri wangu huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Walimu wanaopata ajira wanapangiwa sehemu ya mbali na Wilaya, wanapata shida kufuata malipo yao. Pamoja na hayo, wanapokwenda kufundisha mishahara wanakatwa hapo na nauli anakuwa amejikopa na pesa hakuna. Sasa ninachoomba, Walimu wanapewa ajira na kupelekwa kwenye Wilaya wapewe na mishaara ili iwasadidie huko wanakokwenda kuanza maisha, hawana nyumba; kama kuna nyumba, hakuna choo; hayo ndiyo elimu bure? Elimu bure iko wapi bila miundombinu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, mtoto wa kike akibeba mimba kama wote ni wanafunzi anafukuzwa wa kike tu. Hiyo ni adhabu ya mtu mmoja. Nashauri wote wapate adhabu hata kama sio mwanafunzi mwenzake, wote wape adhabu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, shule za watoto wenye mahitaji maalum ziko vibaya sana. Mimi nilishatembelea baadhi ya shule hizo, kuna Mgeza Mseto; kuna Mgeza Viziwi Bukoba Mjini. Kuna shida kweli! Vitendea kazi hawana hasa mahitaji maalum yote, hawana kabisa. Naomba Wizara msiwe mnasikiliza Watendaji tu jamani, hata wewe Waziri una muda, uende na Kamati kuzunguka kuja kubaini matatizo yaliyomo kwenye elimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho natoa rai yangu hiyo. Tukirudisha elimu, tutakuwa na utajiri, tumeshatatua matatizo yanayotukwamisha. Huo ndio mchango wangu.