Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Ahmed Mabukhut Shabiby

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Gairo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. AHMED M. SHABIBY: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuwa mmoja wa wachangiaji. Kwanza niunge hoja mkono na niishukuru Wizara hii na niwashukuru Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu pamoja na wote wanaohusika kwenye Wizara hii. Labda na mimi sana sana ni kutoa ushauri na ushauri wangu utajikita katika sehemu za biashara hasa katika wafanyabiashara wa kati na wa chini na hii katika ushauri tu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwanza nitaanza na mashine za EFD kwa sababu tupo kwenye Wizara hii ya Bajeti na Fedha. Hizi mashine za EFD lazima zitafutiwe mikakati katika hawa wafanyabiashara wadogo na hata wale wakubwa ambao wanatumia mashine za EFD. Mashine za EFD sasa zimekuwa kero sasa sijafahamu ni makampuni yaliyopewa hii tender za ku-supply kwa sababu utakuta mtu ana duka dogo lakini ile mashine kila siku ni mbovu na sasa imekuwa ni mataji kwa wale watu wenye mashine, utakuta sasa unatakiwa ubadilishe mashine leta hela nyingine, uiboreshe lete pesa nyingine. Sasa hii imekuwa tatizo kwa wafanyabiashara kwa hiyo zingaliwe upya. Hawa-supply au model ya hizi mashine zinazotumika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kitu kingine ni kwenye biashara ya transportation na hasa malori, mimi sina malori. Lakini nafikiri uchunguzi haujafanyika kwa kina kwamba sasa hivi tunazidi kupoteza Watanzania wote ambao wanafanyabishara ya transportation ya malori. Mheshimiwa Rais pamoja na sisi Wabunge tulijitahidi sana wakati ule wa VAT na ile single customer ili bandari yetu ifanye kazi, lakini sasa hivi bandari yetu inafanya vizuri sana, custom pale wanafanya vizuri sana, lakini transportation yote wanafaidika watu wa nje Burundi, Zambia na Rwanda.

Mheshimiwa Spika, watu hawalifahamu lakini sasa hivi magari yote ya Watanzania yanasajiliwa Zambia, Rwanda Burundi na Uganda. Ukitaka kufanya uchunguzi huo kaa barabarani zikipita gari za transit nne; tatu au mbili zina namba ya Rwanda, Burundi au Uganda au Zambia na kwa ushahidi zipo gari zinakuja mpya gari 100/gari 50 zinaenda Zambia zinasajiliwa lakini za Watanzania zinakuwa namba ya kule, kwa hiyo, kodi yote inalipiwa nchi za nje. Na ukitaka kujua kwa akili nyepesi ukiangalia gari za Rwanda, Rwanda wanatumia left hand drive utaona gari ina right hand drive unajua hii gari ya Mtanzania.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo gari zote za transit sasa hivi zinahamia nchi jirani, tatizo ni nini? Lazima hapa tujiulize hapa kuna shida gani. Nilikuwa naomba watu wa TRA hasa ndugu yangu aliyepewa ukamishna sasa hivi kwa sababu najua ni msikivu, ajaribu kukaa na hawa wafanyabiashara angalie kuna shida gani hadi watu sasa wanahama kupeleka kodi kwenye nchi zingine na nilikuwa nashauri sehemu kama hii ni lazima waweke limit kwa mfano kama income tax, najua ukiweka kwenye mambo ya transportation iwe mabasi iwe malori kwamba kodi yetu tukipiga mahesabu kwa jumla ya transportation zote zilizopo Tanzania idadi ya magari labda tunapata kiasi fulani, lakini tuwekea limit kila gari iwe inalipa kiasi hiki najua kabisa mtapata zaidi ya mara kumi ya kodi ya sasa hivi. Kwa sababu wafanyabiashara watanzania ukitaka wafanye hesabu saa nyingine hata tunalaumu TRA, lakini wafanya mahesabu wenyewe wa Tanzania nao ni fake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, unaweza ukawa mfanyabiashara unafanyiwa mahesabu unampekea consultant wa mahesabu anakufanyia mahesabu anaonesha unadaiwa wewe sasa TRA atafanya nini? Wakati huo unayemuamini kwenye mahesabu yeye ndio aliyekufanyia mahesabu anaonesha unadaiwa wewe sasa TRA atakwambia hudaiwi? Kwa hiyo, lazima tuangalie hizi biashara watu wanazozifanya wengi ni watu wa kawaida na watu wa kati. Kwa hiyo, lazima tuangalie namna gani yakuwasaidia na namna gani Serikali itakusanya kodi yake bila kupunguza kodi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitakuja kwenye EFD za kwenye mafuta, hizi ni wizi mtupu kwenye petrol station na wewe nafikiri ni sahidi kwa sababu unafanya hii biashara, hizi ni za wizi na ninajua kabisa Dkt. Mpango, Ndugu Kichere...

MHE. RICHARD M. NDASSA: Kichere hayupo.

MHE. AHMED M. SHABIBY: ... Ndugu Kidata na wote walikuja hawakushiriki katika mchakato wa kuleta hizi EFD walikuta ule mchakato upo, hatuwezi kuwalaumu hao watu.

Mheshimiwa Spika, lakini unanunua lile dubwasha kwa dola 3,000 mpaka 5,000; unalifunga kwenye petrol station kwa mwaka unalipa shilingi 1,200,000 kwa ajili ya yule fundi. Halafu mkoa mzima kuna fundi mmoja, halafu ikiharibika unatoa ripoti TRA kwamba mashine imeharibika, unaendelea kuuza, ile mashine haifanyi kazi, kesho na kesho kutwa anakuja fundi anakwambia kadi imekufa, anachukua shilingi 300,000 kwenye kila pump, yale makaratasi yanayotumika pale ni ya mamilioni kila siku halafu haina faida yoyote kwa sababu EWURA wanatoa bei, tuna chombo cha Serikali kinaitwa EWURA kinajua kabisa mfanyabiashara wa rejareja kwenye kila lita anapata kiasi gani.

Mheshimiwa Spika, kwa mfano mtu anaendesha Kituo cha Engen au Total au Oryx au Gapco au nani anajulikana kabisa kwa lita anapata shilingi 72. Huyo mwendeshaji wa kituo na mafuta yote yanatoka depot. Kwa nini msichukue huko mkate kwenye ile profit ya huyo muuzaji kwa nini msikate pesa yenu huko? Mkatie huko Dar es Salaam kama hii ni shilingi 72 tunachukua tunakata shilingi 15 kwa lita, kusanyeni huko. Kwa sababu mnapotaka kukusanya mafuta yakuja kwa muuzaji wa retail, sasa hivi Wilaya zote kuna boda boda na kuna nini na kuna watu wanauza kwenye mapipa na wanashindwa kudhibitiwa, mtu wanamshushia kutoka kwenye tenki la gari, ana mapipa yake 20 chumba cha 4,500 yanaenda moja kwa moja kwenye mapipa.

Mheshimiwa Spika, mtu ana malori yake, anashusha gereji, haipitii kwenye petrol station, sasa hiyo EFD inafanya nini? Kwa sababu mtu anaamua kuiba anavyotaka yeye, sasa hiyo EFD inafanya nini? Leo mimi nina mabasi, naamua kushusha gereji kwangu na EFD gereji? Kwa hiyo nimechukua mafuta lakini hayakupita kwenye EFD nataka kumuuzia mtu anaenda kuuza kwenye mapipa natoa kwenye gari direct moja kwa moja mpaka kwenye mapipa, kuna EFD? Napeleka shambani kuna EFD? Kwa hiyo kateni huko angalieni kwamba katika vituo vyote tunapata milioni ngapi na tukikata hapa huku basi hatupotezi wala hatupunguzi yale mapato tunayopata.

SPIKA: Mheshimiwa Waziri wa Fedha ukilichukua hilo utapata hela nyingi sana, hizi EFD machine yaani ni kupoteza muda tu kabisa kabisa. Endelea Mheshimiwa Shabiby. (Makofi)

MHE. AHMED M. SHABIBY: Mheshimiwa Spika, ndio cha msingi.

SPIKA: Kata kule kule Dar es Salaam upate hela yako.

MHE. AHMED M. SHABIBY: Mheshimiwa Spika, juzi nimekwenda Kiteto unakuta fundi anaambiwa amemuita fundi ana wiki tatu hajafika kutengeneza mashine za EFD wakati kuna njia rahisi kabisa za kukusanya mapato. Halafu sisi tunawashauri na tunasikia kwa wafanyabiashara wenzetu ili Serikali ipate fedha, basi tunaomba muwe wasikivu hata kwenye haya magari wangeamua tunasema labda kila gani fulani linakwenda transit tunachukua kodi yetu milioni mbili au tatu kwa mwaka wewe shauri yako.

Mheshimiwa Spika, sasa utakuta mtu akiwa ana gari nne hafanyi hesabu, analipa labda milioni moja, mwenye gari tano kwenda mbele anafanya hesabu analipa milioni tatu. Mtu akifikia uwezo wa kununua gari huyo ana uwezo wa kulipa kodi. Kuna haja gani ya kumwambia asifanye hesabu au kama mtu anafanya hesabu afanye lakini pawe na bei inayoeleweka kwamba gari hii mtaondoa hata vyanzo vingine sababu ya kutoa rushwa si kukamata. Hata uweke wakamataji wawe wa wangapi utakamata wote? Sababu ya utoa rushwa ni kutoa vyanzo vya rushwa, kwamba nini kinasababisha hapa ndio unatoa rushwa. Kwamba hiki kinasabaisha rushwa tukiweke mazingira kitakuwa hakina rushwa, hiki kina sababisha kero hii tukiondoa kitakuwa hakina kero, lakini tusitegemee TAKUKURU, TAKUKURU atakamata watu wangapi? Hii kitu haiwezekani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, haya kuna ile watu hapa mwaka jana ilifutwa ilikuwa milioni tatu sijawahi kufanya hiyo. Wala kwa mimi siipendi kuweka jina langu kwenye gari, lakini kuna watu wanapenda kuweka majina kwenye magari, unakuta mtu anaandika King Musukuma, nitolee mfano Musukuma gari yake imeandikwa King Musukuma alikuwa nalipa shilingi milioni tatu lakini wakaja wakapandisha, sasa mwingine haweki lile jina la kwenye plate namba kwa sababu labda ni starehe. Mwingine ana kama akina dada hapa Wabunge na wadada wengine walioko mtaani gari zao wanazitumia vizuri ana TZB hataki hiyo gari ionekane ni TZB anaamua kuandika jina lake pale ili afute ile namba gari isijulikane kama ni gari zamani au gari mpya. Kwa sababu gari yake bado ni nzuri. Wewe unaenda unaweka kodi kubwa, sasa hata nikiangalia sasa hivi kama mapato yapo pale pale lakini waliosajili ni wachache, eeh, tuweke bei ndogo watu wawe wengi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna yale bango yalikuwa kwenye malori hatuna sisi viwanda, lakini mabango ya kwenye viwanda hata sasa hivi ukiangalia unasema malori ya bakhresa yako wapi mbona hayapo, malori ya fulani yapo wapi mbona hayapo, sio kwamba hayapo yale mabango yalikuwekewa sijui milioni nne kwa mwaka ukiandika kwenye lori tu kwamba hii bidhaa fulani inauzwa unalipia milioni nne/ milioni ngapi sasa mwishowe watu wameamua kufuta tu wamebakiza magori mawili/matatu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, weka pesa kidogo upate mapato mengi. Kuna hii...

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Nimekuongeze dakika kidogo endelea Mheshimiwa Shabiby. (Makofi)

MHE. AHMED M. SHABIBY: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Kwa hiyo, utakuta tunachotakiwa sisi kufanya tusizungumze sawa tunasema kwamba kuna biashara zimefungwa labda 1,000 zimefunguliwa biashara 14,000. Lakini biashara zilizofunguliwa 14,000 na zilizofungwa zipo sawa? Inawezekana biashara wamefungua 14,000, 12,000 lakini biashara za briefcase, mtu akenda BRELA kasajili, kaenda TRA kachukua clearance, kaenda Halmashauri kachukua leseni, kafungua biashara, lakini hata duka lenyewe hana. Ukingalia biashara zinazofungwa na zinazofunguliwa na kero nyingine haijatajwa kwenye bajeti hii watu tumeng’ang’ania kero za TRA, lakini kuna watu wengine wana kero kuliko hiyo TRA.

T A A R I F A

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Taarifa Mheshimiwa Susan.

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante naomba nimpe taarifa mzungumzaji Mbunge Mheshimiwa Shabiby kwamba anasema kwamba biashara za kuandika bango na hii imepoteza hela nyingi sana katika nchi yetu kwa mfano mtu ana salon yake akiandika bango ama hoteli wanam-charge hela nyingi, matokeo yake watu wanafuta. Kwa hiyo biashara nyingi hata sasa hata hoteli, maduka, salon wote wameondoa mabango kwa hiyo TRA wanapoteza hela nyingi sana. Bora wapunguze bei ili hawa watu waendelee kuweka bango katika biashara zao. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Shabiby ilikuwa ni taarifa kwako tu.

MHE. AHMED M. SHABIBY: Mheshimiwa Spika, naipokea kwa sababu ni taarifa ya kujenga na tupo pamoja. (Makofi)

Kwa hiyo sisi tunaishauri TRA na nina uhakika kabisa hata watu wanapoizungumzia habari ya TRA lazima tuseme ukweli. Ukiangalia huko juu kwa Makamishna huko hakuna matatizo kabisa, huku chini na ndio maana Rais alisema. Hapa Dodoma mlikuwa mnashuhudia wenyewe mtu anakwenda anafunga duka anasema hapa kazi tu. Kumbe ana roho mbaya, huyo anakuwa ana roho mbaya na Rais Magufuli tu wala hana kitu kingine, hapa kazi tu tumetumwa, wanasema.

Mheshimiwa Spika, lakini sasa hivi bahati nzuri tunashukuru kuna Meneja wa TRA amekuja mpya hapa Dodoma ameondoa hilo tatizo, kwa hiyo, mimi ushauri wangu ni huo. (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Shabiby.

MHE. AHMED M. SHABIBY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana naunga mkono hoja ahsante. (Makofi)