Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuchangia hoja iliyoko mezani hapo.Naunga mkono hoja ya Kambi ya Upinzani moja kwa moja, 100 percent. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi ni mtaalam wa rasilimali watu na kwa vile ni mtaalam wa rasilimali watu, interest yangu kubwa san imekua kwenye upande wa rasilimali watu.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyozungumza mara ya mwisho kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma kuhusu watumishi, ninaendelea kusisitiza kwamba katika awamu hii watumishi wamesahuliwa kabisa. Wamesahauliwa kwa sabbau katika maslahi yao, increment zao za mwaka hawapewi, vilevile hata ile nyongeza ya Mei mwaka juzi imepita, mwaka jana imepita na mwaka huu imepitra bila nyongeza yoyote ya mshahara wakati tunajua kwamba hali ya uchumi imekuwa ni ngumu, vitu vimepanda bei, kama nilivyosema na sasa nasema kwa mfano, kibaba cha unga cha kilo tano ulikuwa unanunua kwa shilingi 2,000 sasa unaunua kwa shilingi 6,000 na mshahara wa mtumishi umebaki pale pale.

Kwa hiyo, ninazidi kusisitiza kwamba watumishi wa umma kwanza ndiyo walipa kodi wazuri, kwa sababu wao wanalipa pay as you earn, wanapopokea mshahara wanalipa kodi ambayo hawawezi hata waka-forge, kwa hiyo, wanailipa kodi stahiki. Kwa mfano, mwaka huu tunategemea pay as you earn itakuwa 1.0 trillion tofauti na mwaka jana ambayo ilikuwa bilioni 998; kwa hiyo, tunaona jinsi ambavyo watumishi wa umma wanachangia kwa kiasi kikubwa katika mapato ya nchi yetu, lakini hatuoni ni kwa jinsi gani na wenyewe sasa wanasaidiwa kufanya maisha yao yawe rahisi kwa sababu wanachangia 67 percent ya kodi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimeangalia bajeti Mheshimiwa Waziri ametenga kama shilingi trilioni saba kwa ajili ya mishahara, kwa hiyo hii itakuwa ni mishahara hakuna hata nyongeza ya mishahara kwa ajili ya watumishi. Sasa mimi ninasikitika sana kwasababu watumishi ndiyo engine ya Serikali, leo watumishi wakiweka mgomo hapatatosha hapa, hakuna kitu kitaendelea, nchi yote itazizima, itasimama. Ni kwa nini Serikali ya Awamu ya Tano haioni umuhimu wa watumishi na kufanya maisha yao yawe rahisi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ni kwa nini sasa kwenye hii pay as you earn Serikali ya awamu ya Tano ionyteshe huruma, ionyeshe interest ya watumishi kwa kuwapunguzia kodi ya pay as you earn? Naomba Mheshimiwa Mpango atakapokuja atuambie ni jinsi gani sasa waonyeshe good will kwa ajili ya watumishi ambao wanaitumikia nchi hii na kuindesha Serikali yenyewe kwa kuwapunguzia kodi ya pay as you earn.

Mheshimiwa Spika, nakuja tena kwenye suala la watumishi; watumishi wanaidai Serikali karibu shilingi bilioni 61 hii ni walimu pamoja na watumishi wengine. Wanadai nyongeza za mshahara, wanadai pesa za likizo, wengine perdiem, Serikali ikikudai itakukata mshahara, ukichelewa kulipa kodi ya ardhi utalipa interest, lakini inakuaje Serikali watumishi wanawadai pesa zote hizo watawapa interest kiasi gani? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa kweli ni jambo la kusikitisha na mimi ninayo mapendekezo ambayo naishauri Serikali ili kuepuka hii adha ya malimbikizo kila siku ya madai ya watumishi miaka nenda miaka rudi, ni muhimu sasa katika pesa zile ambazo ni shilingi bilioni 666 ambazo zimetengwa kwaajili ya kulipa madeni yaliyohakikiwa basi Serikali ihakikishe hayo madeni yanalipwa, hilo moja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili; Serikali ifanye kazi ya ziada kuangalia ni mifumo ipi na taratibu zipi zinazofanya malimbikizo ya madeni na kuna namna ya kufanya. Namna ni kuangalia mfumo wenyewe unavyokwenda. Tunao wataalam wa kuchambua systems, tunaita process analysis. Tutafute watu wa process analysis watufanyie waone ni kitu gani kinachofanya haya madeni kila siku yanalimbikizwa katika Serikali na kufanya ulipaji unakuwa mgumu. Inakuwa ni rahisi kama nyongeza ya mshahara inachukua process mara moja unalipa pesa kidogo kuliko kuwa na malimbikizo kila mwaka inakuwa ni vigumu sana kulipa.

Kwa hiyo, nashauri watafutwe wataalam kama hatunao pale utumishi kwenye Ofisi ya Management Services tulete watu kutoka nje watusaidie kufanya uchambuzi wa huu mfumo ambao unaleta malimbikizo ya madeni. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna tatizo moja pia kubwa ambalo mimi naliona; tatizo kubwa ambalo Serikali inatakiwa kulifanyia kazi ni mfumo wa usimamizi na ukaguzi. Kila mara tunakuwa kama tunastushwa ni kwa sababu hatuna mfumo wa usimamizi na ukaguzi endelevu ambao utaweza kugundua matatizo haraka na kuyashughulikia haraka.

Mheshimiwa Spika, mimi pia napendekeza kwamba uwepo mfumo wa uwajibikaji, kwa watendaji, watendaji wanaohamisha watumishi wakijua hawana bajeti ya kuwalipa wawajibishwe, watumishi wanaoweka taarifa fake kwenye mtandao wawajibishwe na tutakapokuwa na huo mfumo wa kuwajibisha basi tutajenga mfumo ambao ni mwenye integrity, ambao unaweza kufanya kazi vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia ninakwenda kwenye suala la Ubalozi, Balozi zetu hali ya Balozi zetu ni mbaya sana nikiangalia Balozi ya Brussels ambayo jengo sasa karibu litakuwa condemned na inahitajika Euro 300,000 kuweza kulikarabati lile jengo liweze kukaa vizuri, basi katika pesa zile zilizotengwa priority ipewe lile jengo la Brussels ambalo linakutaka kuwa condemned.

Vilevile sisi kama Watanzania tunayo sifa duniani, lakini kama ikiwa tuna viwanja ambavyo tumepewa miaka nenda miaka rudi kujenga Balozi na hatujengi. Tuna kiwanja pale London kimeota magugu kinataka kuwa condemned kile kiwanja, ni kwa nini Serikali haiwezi kutumia mfumo wa mortgage financing kuweza kujenga Ubalozi wetu pale ukafanya hata biashara ukaweka na maduka na nini na ile pesa ambayo inalipwa kila mwaka. Kila mwaka zinalipwa bilioni 21 kwa ajili ya kulipa pango, kwa nini tusifanye mortgage financing na hizo pango zikatumika kulipia madeni ya benki. Mimi sijaelewa ni kwa nini, tuna kiwanja Oman miaka nenda miaka rudi. Tunaomba tutumie mortgage financing, ahsante. (Makofi)