Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia
,bajeti ya fedha ni muhimu sana.

Kwanza nianze na kumpongeza Waziri pamoja na Naibu Waziri na watumishi wote wa Wizara ya Fedha kwa bajeti hii nzuri. Mimi ni mjumbe wa Kamati ya Bajeti, mambo mengi sana nimeshachangia wakati nilikuwa kwenye bajeti kule kama ni ushauri nilitoa kwa speed kubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi niishukuru sana Serikali kuna point moja ambayo imegusa wananchi hasa ile ya kufuta ada ya visima virefu ambavyo vimechimbwa majumbani, hiyo itasaidia sana wananchi kuweza kupata maji kwa sababu wananchi walio wengi wamechimba visima vya maji, sasa vile visima vinawasaidia sana katika matumizi ya nyumbani, kwa hiyo Serikali imeliona hilo na imefuta ada na mimi naishukuru sana Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mmetenga shilingi trilioni 12 kwa ajili ya maendeleo hilo ni jambo jema sana ambayo ni sawa sawa na asilimia 37. Mimi ombi langu nijikite kwenye Jimbo langu la Mufindi Kusini; Jimbo la Mufindi Kusini tuna tatizo kubwa sana la maji na bahati nzuri sana Serikali kila mwaka kuna jambo inafanya kule siyo kwamba Serikali imeniacha kwenye Jimbo langu, kwa mfano Serikali ilitoa shilingi milioni 800 kutekeleza mradi wa Kata ya Itandula pale katika mradi ule matenki yalishajengwa tayari, miundombinu ilishajengwa tayari, tatizo kubwa wananchi bado hawapati maji kwa uhakika na mradi upo na Serikali ilipeleka fedha pale.

Naomba Serikali kufuatilia kwa mfano kwenye vipaumbele vyako umesema mtafanya ufuatiliaji hili nimeona jambo la msingi sana, mtafanya ufuatiliaji kwa kuhakikisha kwamba zile fedha ambazo mnatoa kwenye miradi mikubwa, na kuangalia value for money na imetumikaje na miradi inafanya kazi na wananchi wananufaika

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine kwenye miradi ya maji kwenye Jimbo langu ya Mufundi Kusini miaka ya 1980 mpaka 1990 kuna Kata nyingi sana zilijengewa matenki ya maji, kwa mfano hiyo Kata ya Itandula kuna tenki la maji kubwa sana. Sasa hivi lina zaidi ya miaka sita halifanyi kazi, kuna tenki la maji lingine liko pale Igohole kuna zaidi ya miaka 10 halifanyi kazi, kuna tenki lingine la maji liko pale Nyororo lina miaka karibu mitano halifanyi kazi, kuna tenki lingine la maji liko pale Idunda kuna miaka sita halifanyi kazi, Mtambula pale kuna tenki la maji halifanyi kazi, Ihomasa pale kuna tenki la maji halifanyi kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, haya maeneo niliyoyataja na fedha imeshatengwa tayari kwenye hizi shilingi trilioni 12 naomba tukatengeneze ile miundombinu na tukishatengeneze ile miundombinu naiomba Serikali kama ilivyoandika kwenye vipaumbele ifanye ufuatiliaji kuhakikisha kwamba zile fedha zimetumika vizuri na matenki yale yametengenezwa na wananchi wanafaidika na maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, pale Nyororo mmeshatoa shilingi bilioni 1.4 kwa ajili ya maji pale Nyololo bahati nzuri na tender tayari imeshatangazwa, naomba speed iongezwe yule mkandarasi aweze kufanya kazi pale na wananchi waanze kupata maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nishukuru tena pia kwa kutenga kwenye kulipa madeni ya watumishi hili ni jambo jema sana, kuna watumishi kweli wadai hasa walimu. Sasa nimeona hapa umetenge karibu shilingi bilioni 600 kwa ajili ya kulipa watumishi hili ni jambo jema sana. Kwanza nashangaa kuna watu wengine wanasema Waziri Mpango yaani wanao kama ha-fit pale.

Sasa nataka niwaambie Waziri Mpango hapo ndio mahali pake. Wewe usisikitike kwanza wewe una Ph.D ya uchumi sasa angalia mtu anayekuuliza yeye ana nini? Ana hiyo Ph.D? Rais hajakuweka hapo ameangalia kichwa, ukienda kwa Naibu Waziri nae ni Ph.D holder ni Ph.D. Ndio maana kila sehemu hapo ukiangalia amegusa mwaka jana tulikuwa na Bajeti ya shilingi trilioni 32 sasa hivi shilingi trilioni 33 na ongezeko hili linatokana na mahitaji ya wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mradi mwingine mkubwa sana huu mradi wa umeme, kuna mradi mwingine wa umeme ambao Mradi wa Rufiji sisi hapa tunalalamika umeme sasa hivi hata kwenye jimbo langu watu wanataka umeme, sasa tusipowekeza kwenye umeme Mto Rufiji tusipo wekeza bahati nzuri umetengea shilingi trilioni 1.44 kwa ajili ya kutengeneza huo mradi wa umeme na hilo ndio kufikia mwaka 2020 wananchi wataimba haleluya kwa sababu utakuwa ume-solve problem. Sasa kuna watu wengine vitu kama hivi tukisema maisha bora kwa wananchi, maisha bora wananchi wanataka nini?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza wanataka maji, pili wanataka umeme, tatu wanataka barabara, nne wanataka miundombinu ya afya ikae vizuri. Hivyo ndio vitu vya msingi kwa wananchi na ukisema maisha bora wananchi wapate hivi. Tukiimarisha hospitali zote, zikaa vizuri katika nchi hii, tukaimarisha vituo vya afya, tukaimarisha zahanati, tukaweka miundombinu ikikaa vizuri haya ndio maisha bora kwa kila mtu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza Serikali kwangu kwenye jimbo langu tumemaliza kituo cha afya pale Mahalangali ni kituo kikubwa sana, kikubwa sana na Serikali ilishapeleka shilingi milioni 400 pale. Sasa ni ombi kwa Serikali tukisema value for money ukijenga kituo je, kinatumika? Naiomba Serikali ikafungue kituo kimeisha tayari, peleka vifaa pale vianze kutumika.

Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba Serikali imenipatia shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya kujenga hospitali katika Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, sasa hizi watu wapo site. Lakini niiombe tena Serikali ile shilingi bilioni1.5 haitoshi, naomba Waziri wa Fedha niongezee shilingi bilioni tatu nimalizie hospitali ile ikae vizuri hapa. Naomba uindike kabisa Wilaya ya Mufindi Halmashauri ya Mufindi uniongezee shilingi bilioni tatu iwe hospitali ya mfano pale. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Mufindi kwa makusanyo ya mapato kwenye tano bora tupo; ukikusanya vizuri na matumizi yawe vizuri, sisi tunakusanya vizuri basi mtupatie na matumizi yawe mazuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye barabara; Rais alipokuja tulimuomba tukasema tunaomba barabara kutoka Mafinga kwenda Mgololo iwekwe kiwango cha lami. Kuna barabara kutoka Nyororo mpaka Mtwango iweke kiwango cha lami, na hizi barabara zipo kwenye ilani ya Chama cha Mapinduzi nilivyomwambia anasoma hapa kwenye bajeti ameweka tayari katika barabara kuu zitakazowekwa kiwango cha lami mojawapo ni ya kutoka Mafinga mpaka Mgololo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Waziri Mpango nimekushukuru sana kwa hii barabara kuiwekea lami, ni barabara muhimu mno kwa uchumi, ukisikia viwanda vipi kule, kiwanda cha karatasi kipo kule, kiwanda cha chai kipo kule, kiwanda cha mbao kipo kule. Sasa tayari unaanza kujenga kiwango cha lami, excellent kilometa kama tatu umeshajenga na hivi utaendelea. Sasa kuna mtu anasema akutoe wewe unayenipangia bajeti nzuri kwangu. Bajeti imekaa vizuri pale kwangu tayari. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tukitengeneza barabara zikaa vizuri kuna barabara ya kutoka Sawala mpaka pale Mninga hiyo ni ya kata, ulinijengea kilometa 14 kiwango ha lami, imeakaa vizuri wananchi wanapita pale, wapo vizuri kuna barabara kilometa 33 kutoka Sawala mpaka Nyegea iko kwenye mpango na upembuzi yakinifu ulishakamilika. Hawa ni wafadhili, Serikali kazi na kutafuta wafadhili tunaweka kule, wamekaa vizuri. Sasa kwenye jimbo langu la Mufingi kusini nikijenga barabara ya kutoka Malangali mpaka Kwatwanga mpaka Mbalamaziwa; nijenga barabara ya kutoka Nyororo mpaka Mtwango, nikijenga barabara kutoka Mafinga mpaka Igohole, nikijenga barabara ya kutoka Mgololo mpaka kule Njigo, nikijienga barabara ya kutoka Nyororo mpaka kule Maduma, nikijenga barabara kutoka Sawala mpaka Iyegewa, nikijenga barabara Mninga mpaka Mtambula; hizo barabara Serikali ikizijenga basi jimbo langu lile litakuwa limekaa vizuri.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mitandao ya barabara ndani ya jimbo wananchi wa uwezo kufanya kazi za kila siku na uchumi kupanda. (Makofi)