Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Spika, ahsante nashukuru kwa kunipa nafasi hii nitakuwa na machache.

Mheshimiwa Spika, la kwanza kabla sijasahau ningependa Mheshimiwa Waziri wa Fedha atakapokuja atueleze zile kodi zinazodaiwa (tax refund) kwa mwaka mmoja kwa sababu kuna mashirika mengi na baadhi ya mashirika ni yale hata Serikali yenyewe ina hisa, lakini wanadai tax refund. Ningependa Waziri aje na figure atueleze angalau kodi ambayo TRA wanapaswa kui-refund kwa wafanyabiashara na makampuni ni kiasi kadhaa. Kwa hiyo, nilikuwa naomba hilo kabla sijasahau.

Mheshimiwa Spika, nina mawili madogo tu, la kwanza ningependa sana sana hayo yaliyozungumzwa jambo ni moja ni menejimenti ya uchumi wa nchi yetu. Bahati nzuri Waziri wa Fedha na Naibu wake ni wataalam wa masuala haya, ukisikiliza michango ya Wabunge yote hata Wapinzani wetu walivyosema ni kwamba lipo tatizo la msingi la economic management ya uchumi wa nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, hili jambo ushauri wangu mambo ni mengi na nchi ni kubwa. Nchi hii lazima tu-source talent za wenye uwezo mkubwa. Kuna watu wana uwezo mkubwa katika nchi yetu. Watu kama akina Profesa Ndulu kwa mfano, natoa mfano watu kama wakina Mafuru yule aliyekuwa TR kwa mfano na wengine wengi wapo wengi ndani ya CCM na nje ya CCM. Watu ambao tunaweza tukawafanya kama think tank ya nchi yetu wakamsaidia Waziri wa Fedha katika ku-manage uchumi wa nchi hii yako mambo mengi, mengi ambayo nina hakika yangetuletea fedha nyingi sana katika nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, maana hapa shida ni kwamba uchumi ni mdogo, sungura ni mdogo lakini bado vipo vyanzo vingi sana fedha ambavyo havijaguswa, kwa mfano, chukua item moja uvuvi wa bahari kuu, alikuja mtaalam mmoja kutoka Zanzibar, alikuwa Mzanzibar mwenye maarifa mengi sana wakati nipo Kamati ya Kilimo na Mifugo. Alitupitisha kwenye uchumi wa bahari kuu, alitushawishi kabisa kwamba kile ni chanzo ambacho hakijaguswa kabisa. Kwa sababu kuna nchi zinaendeshwa kwa kodi ya uvuvi wa baharini Seychelles, Maldives ni nchi ambazo zitegemea uchumi wa bahari kuu, lakini sisi hatuzungumzi na hata kwenye kitabu husikii kama Waziri wa Fedha anazungumza kama kuna source revenue nyingine muhimu sana ambayo imejificha kwenye bahari yetu.

Mheshimiwa Spika, ningeshauri sincerely bado kabisa kwamba Waziri wa Fedha una mamlaka kwa mujibu wa instrument yako unda timu ya wataalam, wazee kama kina Mzee Ndulu wakushauri mambo ya msingi yakufanya.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili ambalo ningependa nizungumze ni haya mashirika na makapuni ambayo Serikali zina hisa. Tuchukue mfano hivi Kampuni kama Kilombero Sugar Company, kama TPC, Kampuni kama Puma Energy hivi Serikali ina maximize hisa zake zilizopo kule? Ni mambo ya kujiuliza tu. Sisi tulitembelea wakati nipo Kamati ya Kilimo tulitembea Kilombero Sugar Company, tukakuta pale kuna hisa kubwa za Serikali; 25% ya hisa za Kilombero Sugar Company ni za Serikali. Ukienda TPC 30% ni za Serikali na ukienda Puma Energy 50% ni za Serikali, lakini kweli Serikali ina maximize?

Mheshimiwa Spika, nafikiri wakati umefika Msajili wa Hazina ifanye kazi yake kwa umakini mkubwa ili mashirika haya ambayo Serikali iliwekeza hisa zake yaweze kuwa faida. Mheshimiwa Waziri Mpango naamini ile dividend ya bilioni ya tano/bilioni saba/bilioni mbili/milioni 500 ni kidogo mno. Naamini kabisa haya mashirika na yapo mengi kweli kweli yapo mengi tunapata kidogo sana ukilingaisha na investment ya hisa Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukianga dividend ambayo inalipwa njoo kwenye kodi malipo ya kodi, njoo kwenye ajira na Mheshimiwa Jenista wewe ni Waziri wa Ajira, jambo lingine kubwa katika nchi yetu ni suala la ajira jamani. Suala la employment ni jambo kubwa sana, ni jambo kubwa, vijana wanatoka vyuo vikuu na wote tunaona kwamba ni mambo ya kawaida.

Kwa hiyo, mashirika hayo mwenyekiti yapo mengi yapo zaidi ya 200 na mimi na hakika bado mchango wake kwa uchumi wa Taifa letu, mchango wake kwa pato letu, mchango wake kwenye Mfuko wa Hazina bado ni kidogo ni kidogo ni kidogo sana.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili ambalo ningependa nilizungumze ni jambo la TRA. Nashukuru nah ii tunamshukuru Mheshimiwa Rais mwenye ndio ameingilia kati kwamba TRA wawe marafiki wa wafanyabiashara, otherwise ilikuwa imefika mahali sasa TRA kazi yao ni kuwinda wafanyabiashara. Na rafiki yangu ana kiwanda kule Arusha alifuatwa na bunduki na polisi wakachukua computer zake na maskini ya Mungu akaamua kuacha biashara ame- reallocate amekwenda Jinja nchini Uganda.

Mheshimiwa Spika, sasa angalau tunaona TRA wameanza angalau kuwa marafiki wa wafanyabiashara, hiyo inatutia moyo na TRA sasa waende na trend hiyo, kwamba kazi ya TRA iwe ni ya kukusanya kodi na kamwe wasiwe maadui wa wafanyabiashara na wewe responsible kwa wafanyabiashara, wawasikilize wafanyabiashara, bila wafanyabiashara hawa kusaidia uchumi wa nchi hii tutapata matatizo na hatuwezi kujidai kwamba nchi itakwenda yenyewe bila kuwa na private sector na bila kuwa na hawa wafanyabiashara. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ambalo ningependa nitoe angalizo kwa Wizara ni matumizi makubwa ya Serikali. Ninaamini bado Serikali ina matumizi ya hovyo na makubwa sana. Kwa mfano, hivi nchi maskini kama hii nchi inayoendelea kama hii inawezaje ku-afford misaada ya Serikali inanunua magari ya kifahari ndio wanayotumia watendaji wetu ambapo maskini wanapaswa watumie magari ya kawaida kabisa. Unakuta gari shangingi, Vx 8, DFP iko Kasulu kule, mambo ya ajabu kabisa haya.

Mheshimiwa Spika, huko nyuma ilikuwa mkazo na trend ni matumizi ya Serikali hovyo ya Serikali ili fedha nyingi kama anavyosema Mheshimiwa Rais Magufuli tuzipeleke kwa watu tukajenge vituo vya afya tukajenge shule zetu na kadhalika na kadhalika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini Mheshimiwa Waziri bado yapo matumizi ya hovyo ya magari ya anasa kabisa ambayo hajapaswi kuwepo katika nchi yetu. Ukienda Uganda na nilibahatika kwenda Uganda mwaka jana tulikweda kwenye ziara ya wakimbizi. Ukienda Uganda hawana trend hiyo, hiyo luxury hiyo wameshaiacha. Hatusemi watembee na baiskeli Mheshimiwa Jenista no, no hoja sio hiyo, hiyo ni kupotosha hivi kwa mfano una mpaje Regional Manager wa TANROADS shanging Vx 8 why?

Mheshimiwa Spika, Regional Manager wa TANROADS kwa nini usimpe a good pickup car akikuta bango la barabara limeanguka, akatoka kwenye gari yake, akachukua bango lake, akaweka kwenye gari yake nimetoa mfano mgodo tu. Kwanini umpe Vx 8 nani ana service gari ile? (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, hoja ya msingi ni kwamba Mheshimiwa Waziri nenda kaangalie kwenye archives yako bado matumizi ya hovyo ya Serikali ni makubwa sana na Serikali ina kazi nyingi sana za kufanya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la mwisho nikukumbushe Mheshimiwa Waziri, sisi Halmshauri ya Mji wa Kasulu tumeshatoa kiwanja kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya TRA, kwa maana ya Buhigwe na Kasulu tumetoa kiwanja bure kwa TRA kujenga ofisi zake na mwaka wa jana uliniahidi kwamba TRA wataanza kujenga ofisi pale na kile kiwanja tumewapa bure, sasa mambo mawili au mnajenga au hamjengi turudishieni kiwanja chetu tukitumie kwa mtumizi mengine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimshauri Waziri wa fedha afanye ziara katika Wilaya ya Buhigwe na Kasulu ajionee hali halisi yamambo yalivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada kusema hayo nakushukuru naunga mkono hoja hii, ahsante sana. (Makofi)