Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Spika, ahsante labda na mimi nianze kwa kumshukuru Mwenyezi mungu kwa kutujaalia kuwa katika Bunge letu hili tukiwa na afya njema.

Mimi niseme tu kwamba pamoja na kumpongeza Mheshimiwa Waziri, lakini bado hali yetu ya maisha Watanzania ni ngumu hususan ukiangalia hali ya kiuchumi kila siku inaendelea kuwa ngumu na maisha katika Tanzania kila ni afadhali ya jana na hii inatokana na nini kwanza mazingira kibiashara na kodi sio rafiki na hili nalisema kwa sababu ukiangalia tuna tofauti kubwa na wenzetu.

Sisi watanzania unaanza kulipa kodi kabla hujafanya biashara, ukitaka kufungua biashara kwanza upate TIN Number, uende TRA wakufanyie assessment, kabla ya hili halijafanyika unaanza kulipa sasa inakuwa ni taabu na hususan niende kwa akina mama, akina mama wengi ni wafanyabiashara wadogo wadogo, wajasiriliamali, wenye maduka ya nguo, wenye maduka ya vyakula, lakini wanapata tabu hali ya kuwa kwanza hata mikopo wanapochukua msharti ni magumu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa hili naliona ni tatizo kubwa kibiashara ukinagalia baadhi ya nchi jirani kama Kenya, labda Rwanda au Uganda wenzetu wafanyabiasha wanapaanza wanapewa tax holiday ya karibu miezi sita angalau wajiimarishe waweze kujua faida wanapata vipi na aangalie mtiririko wa biashara unaendaje, lakini kwetu ni tofauti. Sasa nashauri Mheshimiwa Waziri jambo jema huigwa, hebu tuige wenzetutuwasidie wafanyabiasha wetu wadogo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, yamesemwa maneno mengi hapa na wenzangu, lakini kiukweli hata ukija kwenye mfumuko wa bei tunasema tu kwamba mfumuko wa bei umepungua kwa 3.9%. Lakini h ivi tuulizane Wabunge ni kweli mfumuko wa bei umepungua? Twende kwenye petrol na diesel tunayoitumia mwaka jana ilikuwa takribani shilingi 1800 leo shilingi 2290. Hapa mfumuko wa bei umepungua au umepanda? Wale tunoafunga tunajua mwaka jana bei ya kilo moja ya tambi ilikuwa shilingi 1800 leo shilinig 2500. Maharage yalikuwa kilo moja shilingi 1700 leo shilingi 2400, sukari ilikuwa shilingi 1900 au shilingi 2000 leo shilingi 2500. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa mwananchi wa kawaida unapomwambia kwamba mfumuko wa bei umepungua hakuelewi hata tukienda kwenye shilingi yetu ta Tanzania kila kukicha thamani ya shilingi ina shuka. Tujilinganishe na Kenya, tujilinganishe na dola ya Marekani hela yetu inazidi kupungua thamani kila uchao, lakini tunasema uchumi unakuwa pato na Taifa linaongeza, lakini mwananchi wa kawaida mtaani ukimtanzama amechoka hohe hahe, hajielewi kabisa yaani haelewi somo.

Mheshimiwa Spika, sasa mimi niseme tunaponzungumza mambo mengine tuwafikirieni hawa watanzania wenzetu ambao asilimia kubwa wapo vijiji na mijini na ambapo wengine hawana hata ajiri unapomwambia mtu uchumi umekuwa hata hakuelewi. Kwa hiyo, niseme hebu tuwaeleze ukweli lakini vilevile pia tuwaweke mazingira rafiki ya biashara kwa sababu wafanyabiashara wengi sasa hivi wanalalamika.

Mheshimiwa Spika, juzi hapa nilikuta Katibu wa Chama cha Biashara Mkoa wa Tanga ananiambia Mheshimiwa kutokana na ukali wa kodi nina barua 60 za wafanyabiashara ambao wanataka kufunga biashara wanaandika barua TRA ili wasidaiwe tena kodi. Sio Tanga tu, Dar es Salaam leo ukitaka frame katikati ya Jiji Kariakoo leo unapata. Kwa sababu gani watu wanashindwa kufungua biashara, mzunguko wa fedha umekuwa ni mdogo biashara zinafungwa na mwaka jana nilishauri hili Mheshimiwa Waziri alisema katika moja ya mafanikio Wizara ni kwamba wamefunga biashara takribani 300 kwa Dar es Salaam. Na nilisema kufunga biashara sio mafanikio kwa sababu kila biashara moja uliyoifunga pana wafanyakazi labda hao kwenye duka ua kampuni hao wanategemewa na watu 11 mgongoni, sasa unaposema umefunga biashara kwanza tunakosa mapato, lakini pili tunateketeza familia za Watanzania.

Kwa hiyo mimi niseme kufunga biashara kodi kubwa sio mafanikio ni matatizo watu hawana ajira Tanzania wanakimbilia kwenye biashara. Kwenye biashara napo kodi kubwa wakienda kwenye kilimo ndio hivyo, kwenye korosho kuna matatizo, sasa tunaelekea mpaka kwenye mahindi.

Mheshimiwa Spika, amezungumza hapa Waziri wa Kilimo kwamba wenye mahindi mengi wampe taarifa. Lakini watakapokuwa wemeleta hiyo taarifa kodi itapungua? Hawawezi kutoa taarifa kwa Waziri wa Kilimo kwa sababu wanajua nikisema nina tani 50 za mahindi tayari TRA watanikalia benet, hawawezi kukupa, lazima tupunguze kodi nafikiri wajua katika commerce kuna the law of demand.

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Mbarouk.

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Spika, kwamba the low price, high demand and the high price, low demand. Tuweke mazingira hayo angalu tuwasaidie wafanyabishara. Wafanyabiasha hasa sisi wa mikoa ya karibu na mipakani wananchi wetu wanakwenda Kenya, Uganda na Congo kuchukua bidhaa ili waweze kuuza wajipate kipato cha kila siku, ahsante. (Makofi)