Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Peter Joseph Serukamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kucahngia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kabisa kabisa kumpongeza Waziri Lukuvi na Wizara nzima ya Ardhi. Waziri Lukuvi mimi nakuombea heri sana, angalau ni kati ya Mawaziri wachache ukienda ofisini kwake atakusikiliza na utaondoka na jawabu. Mimi huwa najiuliza Lukuvi aidha labda hana kazi sana ama Lukuvi anawapenda Wabunge na anapenda kutatua matatizo. Kwasababu Mawaziri wengine kwa kweli wako busy kweli, ukikutana naye ana haraka na hakusikilizi vizuri. Mheshimiwa Lukuvi mimi naomba niseme nakupongeza sana.

Mheshimiwa Spika, na kwa kiasi kikubwa unaweza ukaona matatizo ya ardhi mengi sana yametatuliwa kipindi hiki cha Mheshimiwa Waziri Lukuvi. Nakushukuru sana Waziri Lukuvi, nawashukuru watendaji wote wa Wizara, Naibu Waziri na Katibu Mkuu kwa kazi kubwa mnayofanya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi nina mambo mawili tu ya kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, la kwanza ni suala la National Housing. Nimesoma hapa ndani kwenye kitabu Mheshimiwa Waziri amesema kuhusu National Haousing. Mimi nataka nikushauri Mheshimiwa Waziri; nadhani umefika wakati National Housing iwe na department mbili. Moja ihangaieke na nyumba kwa ajili ya wafanyakazi wa Tanzania ambao ni kwa ajili ya punagisha, na ndilo lilikuwa dhumuni la Shirika hili. Mbili, kuwe kuna wing ya biashara ya kujenga nyumba kwa ajili ya kuuza. Nina uhakika National Housing wakifanyakazi hizi; lakini mkataka wafanye kazi za nyumba za kuuza, nyumba za kupangisha tunawachanganya na ndiyo maana leo kuna miradi mikubwa sana pale Dar es Salaam imesimama.

Mheshimiwa Spika, ningemwomba Mheshimiwa Waziri, ile miradi tukiiacha isimame sisi tunapata hasara kwasababu wale wakandarasi wako site tayari. Kama hamuwalipi wao wanapata interest, wanapata idle time; kwahiyo at the end of the day looser ni Serikali. Whether mikataba ilikuwa mibaya, whether mikataba ilikuwa ni mizuri lakini it is our interest tuhakikishe tunamaliza kazi za majumba yote ya Dar es salaam; kwasababu Shirika limekopa Benki, Shirika limeweka collateral. Sasa kama hatuwezi kumalizia zile nyumba maana yake hizi collateral zinakuaje? Na leo kinachoonekana kama vile National Housing imendoka na Nahemia Mchechu, that is the vibrancy ya National Housing haionekani. Is it true kweli kwamba ni mtu mmoja ameondoka mabo yamebadilika?

Mheshimiwa Spika, mimi sitaki kuamini hayo, nataka kuamini kwamba ningeomba Serikalini turudi kwenye drawing board, kwanza tumalize yale tuliyoyaanza halafu ndipo tuje na mpango mpya; lakini tukisema tunakuja na mpango mpya yale tuliyoyaanza tunayaacha barabarani kwa kweli tunajichoma wenyewe hatima yake collateral zetu zitaanza kuuzwa; nani atalipa hii gharama? Maana project zikisimama zina-accrue interest, kitakachotokea ni nini? Maana yake gharama ni kubwa na Shirika letu tunaliingiza kwenye madeni makubwa. Kwahiyo niwaombe Serikali kwa umoja wenu nawaombeni tatizo la National Housing tulitatue, tuipe nguvu National Housing ifanye kazi yake.

Mheshimiwa Spika, la pili, nataka nizungumzie suala la mortgage financing. Toka nimeingia kwenye Bunge hili tulitunga Sheria ya Mortgage Financing lakini bado interest za benki ni kubwa sana. Matokeo yake ndiyo maana mortgage financing haishamiri, nchi za wenzetu ukimaliza university ukipata kazi siku ya pili tu ziko nyumba za kwenda kupanga ambazo unauziwa kwa interest unalipa baada ya miaka 20, baada ya miaka 30, namna hiyo tutaweza kuwasadia wafanyakazi wa Tanzania. Kama mortgage financing hii ninayoijua ambayo ni benki zimeamua yao, ambayo interest ni kubwa bado mortgage financing Tanzania safari yetu ni ndefu sana. Ningeomba turudi kwenye drawing body tuangalie hizi interest rate, kama interest rate tuziongezee miaka mingi ya kurudisha fedha nina hakika tutakuwa tumewasaidia wafanyakazi wa Tanzania na Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la mwisho, nataka kuzungumzia suala la Land Bank; marehemu Mzee Mungai aliwahi kusema hapa Bungeni kwamba tunatamba sana tuna ardhi kubwa sana, Watanzania tuna ardhi yetu, Wakenya wanatuonea wivu kwa ardhi yetu, kila mtu anatuonea wivu ardhi yetu lakini ardhi isiyoleta mali ya nini. Leo tuna ardhi tunatamba nayo halafu tunakufa njaa, tuna ardhi tunatamba nayo ukiangalia kwenye GDP growth kutoka kwenye agriculture ni ndogo. Nilitarajia tumepata ardhi hii, iwe ni kichocheo kikubwa cha uchumi wa Tanzania. Kwa nini nasema hivyo? Angalia kahawa Tanzania tunazalisha tani 50,000 nchi nzima hapo Uganda tani 288,000, wana ardhi ndogo kuliko sisi tuna ardhi kubwa lakini hakuna ni kwa sababu gani tunataka kila mtu alime. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hatuwezi kuendelea hatuwezi kuja na commercial farming, kama tunataka kila mtu alime matokeo yake itakuwa ni umaskini tu, mama yangu kijijini analima miaka yote lakini hajawahi kujitosheleza kila mwaka anazo heka mbili, heka tatu zinamsaidia nini, hivyo, ningeshauri Mheshimiwa Waziri Lukuvi umefika wakati tupime ardhi yetu tuwe na maeneo ya ardhi ambayo ni kwa ajili ya large plantations, kwa ajili ya commercial farming, hili ndio itatufanya Tanzania tuilishe East Africa, tuilishe Afrika kwa sababu Mungu ametupa ardhi na ametupa maji. Hata hivyo, kama hatuna mpango miji tunadhani nia yetu ni kila mkulima, kila Mtanzania awe na kipande chake kidogo cha ardhi mwisho wa siku kukitoa draught tutakufa njaa.

Mheshimiwa Spika, yako mazao ambayo tulipaswa Tanzania tuwe tuna read kwenye hilo continent, kwa mfano kahawa tuna eneo kubwa sana tulitakiwa tunashinda Ethiopia. Angalia mkonge tuna uwezo wa kuzalisha tani 1,000,000 za mkonge lakini tunazalisha tani 19,000 na tuna ardhi yote hii, kwa nini? Kwa sababu hatuja-embrace commercial farming, hata kule ambako kuna mashamba tunaseme tuwape watu wadogo yeye si ndio atalima mahindi, kesho anaendelea kuwa masikini tu.

Mheshimiwa Spika, haya kwenye chai tuna maeneo makubwa sana ya land ambayo tunaweza tukalima chai, unajua tunazalisha tani ngapi za chai kwa mwaka, tani 19,000, Kenya tani 3,80,000, hivyo ikitokea bei ya chai imeanguka duniani sisi inatuumiza kwa sababu hatuna economics of scale. Sasa mimi sielewi naomba wenzangu watusaidie.

Mheshimiwa Spika, suala la pareto, suala la korosho, korosho tuna tani 210,000, Nigeria wana tani 890,000, ukiangalia hata ugomvi wetu wote ni kwa sababu tunagombania kidogo tulichonacho, lakini tunayo ardhi ya kuweza kulima na tuka-benefit kwenye economics of scale. Hivyo ningeomba Mheshimiwa Waziri Lukuvi umefika wakati na najua hili analiweza, umefika wakati tutengeneze ardhi hata tukiwatafuta investors wakatuambia nataka ardhi ya kulima kitu Fulani, unamwambiwa ardhi hii hapa.

Mheshimiwa Spika, leo akija investor anataka kulima kwa mfano makademia ambao ni very higher product, kuna Wakenya wanakuja hapa kutafuta ardhi, hawaoneshi lakini tunaimba ardhi tunayo. Kama ardhi hii haituletei maendeleo, ardhi haituletei uchumi, nadhani tunaji-contradict na hakuna maana ya kuwa na hii ardhi kama haiwezi kutuletea maendeleo, kwa sababu ardhi ndio maendeleo ya watu.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)