Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa fursa ya kuchangia.

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kumpongeza mtoa hoja, Mheshimiwa Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi, kwa kuwasilisha Mpango na Makadirio ya Bajeti ya Wizara yake kwa umahiri mkubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitaongelea masuala mawili mafupi tu ndani ya muda huu mdogo nilionao ambayo yamegusiwa na Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani, Mheshimiwa Salome Makamba.

Mheshimiwa Naibu Spika, pengine nianze kwa upande huo vilevile kwa kumpongeza Mheshimiwa Makamba kwa kukiri mbele yetu kwamba nyuma ya mwanamke yeyote mwenye mafanikio yupo mwanaume. Hii ni dhahiri kabisa kwamba ana familia yenye furaha katika nchi hii. Mimi naomba nimkumbushe tu kwamba pale ambapo kuna familia yenye furaha basi nyuma yake kuna Serikali inayojali na Serikali hiyo ni ya Chama cha Mapinduzi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani ametoa picha ukurasa ule wa saba wa nchi yetu kuwa yenye ukandamizaji mkubwa na amenukuu tafiti mbalimbali alizozisoma yeye. Mimi naomba tu nimkumbushe vilevile tafiti ambazo zimefanywa na vyombo vyenye heshima kubwa sana duniani.

Mheshimiwa Naibu Spika, Taasisi inayoheshimika duniani upande wa Travel Advisory, Atlas and Boots, inatoa orodha ya usalama wa nchi duniani kila mwaka inaitwa Global Peace Index. Inasema kwa mwaka 2018 nchi 100 zilikuwa na hali mbaya sana ya usalama.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitangaze hapa na niko tayari kuweka juu ya Meza hapo, kwamba Tanzania haipo kati ya nchi 100 hatari duniani. Nilizoziona humu ni Syria, Afghanistan, Russia, Pakistan, Uturuki, Israeli, Colombia, na USA ni ya 43, sisi kwenye 100 hatumo. USA yenyewe ambayo wengi wanadhani ni paradiso ya usalama ni ya 43. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nchi zilizobaki salama zingine ziko kama 80; Ufaransa (103), Vietnam (104), Uingereza (107), Qatar (108), Tanzania (113) yaani tuko juu ya hata hao. Ndiyo shida ya kunukuu hivi vitu, basi nukuu vyote ili kupata picha comprehensive. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukisoma worldpopulationreview.com inatoa orodha ya nchi 55 za kidikteta duniani, tena 55 imefikia mwisho, Tanzania siyo mojawapo. Kwa hiyo, ukitaka kuleta data hapa uwe comprehensive, jaribu kusoma nyingi uweze kupata picha kamili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, amedai vilevile kuwa kuna ukosefu wa uhuru wa vyombo vya habari Tanzania. Anasema hii ndiyo dosari kubwa kwelikweli hapa nchini. Mimi nataka tu niwahoji wenzangu ambao wanakuja na hiyo hoja mara kwa mara, wanaposimama hapa Bungeni hebu wanitolee mfano wa nchi moja tu yenye uhuru wa vyombo vya habari usio na mipaka, nitafurahi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pengine wanafikiri ni hao wakubwa, sasa kama ni wakubwa, hivi kama wakubwa hawana mipaka ni kitu gani kinawafanya mpaka leo huu mwaka wa saba wanahangaika na Assange? Ni kitu gani kinawafanya mpaka leo wanahangaika na Snowden? Yote ni kwamba wamekiuka ule uhuru wa habari uliopo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwasisitizie Watanzania na Waheshimiwa Wabunge kupitia kwako kwamba nchi zote zenye heshima duniani zimesaini Mkataba wa Civil and Political Rights, ile convention ya mwaka 1966. Convention hiyo inatoa uhuru kwa vyombo vya habari lakini kwa sharti la kwamba usiingilie uhuru na haki ya mtu mwingine na usihatarishe usalama wa nchi yako. Sasa kama unahatarisha usalama wa nchi yako wewe utakaa kwenye nchi gani? Kwa hiyo, ndiyo maana nchi zote zinasema sisi tunafuata uhuru wa vyombo vya habari lakini tunazingatia hiyo International Convention ya Civil and Political Rights. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimalizie kwa kusema tu kwamba Tanzania tunapewa marks kubwa kwa sababu ya utayari wetu na vilevile kuwa champions wa kuanzisha vyombo vya ulinzi wa haki za binadamu. Nimefurahi sana leo Chief Whip hapa ameelezea kuhusu Mahakama zote za Afrika na za kimataifa ziko Arusha kwa sababu ya track record ya human rights ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi ndiyo tulikuwa waanzilishi wa hoja tuwe na East African Court of Justice hapa na Mahakama ya Afrika. Siyo hivyo tu, Mahakama ya Afrika tukawa moja ya nchi tano tu tuliokubali wananchi wetu watupeleke kwenye hiyo Mahakama kama kuna ukiukwaji wa haki za binadamu, tano, kati ya nchi zote za Afrika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)