Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa nafasi na masikitiko yangu ni jinsi ambavyo hotuba yetu imekatwakatwa, lakini naamini kabisa watu wameelewa nini kinachoendelea na imekuwa bahati mbaya sana, mambo haya yanasemwa Mabalozi wetu wapo hapa juu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niendelee. Wizara hii ni muhimu sana na ndiyo kioo cha nchi kwenye dunia au kwenye ulimwengu wetu. Kwa hiyo chochote kinachofanyika ndani ya nchi, Wizara hii ipo responsible na ndiyo sababu umeona kwamba wameangalia Wizara zote kuanzia kilimo na nini na nini na ndiyo sababu hata Kambi ya Upinzani tumeongelea masuala hayo ya kilimo na mengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu kwamba kuna tatizo kubwa sana katika Wizara hii. Nizungumzie suala la watumishi, kumekuwa na tatizo kubwa sana la kupandishwa vyeo, pamoja na kwamba ni tatizo la kitaifa, lakini nilitegemea Wizara hii ingeweza kuwapandisha watumishi wake kwa takribani miaka 12 bado watumishi wa Wizara waliokuwa kwenye cheo fulani kwa mfano ile Foreign Service I mpaka leo kwa miaka 12 walitakiwa wawe Principal Officers lakini bado wako pale. kwa hiyo, naishauri Serikali wafanye kuwapandisha kwa mserereko ili waweze kupata hadhi yao na hivyo kuleta motisha katika kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia pia bajeti; bajeti na nashukuru hata Kamati imesema na Kambi. Ukiangalia mishahara, kwa mfano nimejaribu kuchukua, ukiangalia recurrent budget kwa mwaka jana na mwaka huu utaona kuna tofauti ya takribani shilingi bilioni 10, lakini kibaya zaidi angalia kwenye zile multilateral missions, unakuta kuna upungufu mkubwa sana wa mishahara. Kwa mfano, Balozi wetu wa London mwaka jana kwenye mishahara tu (basic salary) ilikuwa milioni 177, mwaka huu milioni 81. Ukija Lusaka ilikuwa milioni 93, mwaka huu milioni saba, ukienda Moscow ilikuwa milioni 116, mwaka huu milioni 77, ukienda Ottawa Canada ilikuwa milioni 107, mwaka huu milioni 49, ukija Rome ambako ni Multilateral tuna FAO na mambo mengine ilikuwa milioni 166, mwaka huu ni milioni 100, ukija Riyadh ilikuwa 110, mwaka huu ni milioni 81, ukija New York ambapo tuna Mashirika makubwa ya Kimataifa ilikuwa milioni 88, mwaka huu milioni 64.

Mheshimiwa Naibu Spika, hii ina-cut across kwenye Balozi zetu zote na hili ni tatizo kwa sababu tunajua kwamba toka mwaka 2016 walivyorudisha baadhi ya Maafisa wa Ubalozi, bado hawajafanya replacement. Nilikuwa Doha mwaka huu, pale wana watumishi wawili tu, Balozi na mtumishi mmoja au wawili, ukienda New York ni hivyo hivyo, nimetembea nchi nyingi kuna matatizo makubwa ya watumishi. Nataka kujua ni kwa sababu gani baada ya kurudisha baadhi ya watumishi, hawajawa-replace kwenye Balozi hizo kiasi kwamba hii inakuwa reflected kabisa kwenye hii mishahara. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba kumekuwa na tatizo kubwa sana la utendaji na ndiyo maana tunasema sasa ni lazima Waziri anapokuja ku-wind up atuambie baada ya kupunguza Maafisa wa Balozi, ni kazi gani wamefanya kuhakikisha kwamba wanawa-replace ili kazi ziweze kwenda. Tunajua kwa mfano pale New York wameondoa watu wengi sana, kwa hiyo Kamati mbalimbali hazipati watu wa kufanya hizo kazi au mtu mmoja anafanya kazi ya watu watatu. Kwa hiyo, tunaomba na hilo lifanyiwe kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi kama Bunge tuna passport za Kibalozi, lakini na wengine wengi. Siku za nyuma tulikuwa tuna utaratibu mzuri, Chief of Protocal alikuwa anakuja kutoa mafunzo ya etiquettes na ni jinsi gani mtu anaweza ku-appear. Leo hivi tunaona hata Mabalozi wetu hawajui hizo etiquettes; inawezekanaje Balozi wa nchi anafuta miwani kwa kutumia ulimi. Kwa hiyo, haya ni mambo ambayo tunaona hayafai kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana… (Makofi) (Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)