Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru na niungane na Waheshimiwa Wabunge kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na wataalam wetu wa Wizara ya Nishati.

Mheshimiwa Spika, imezungumzwa vizuri juu ya mradi wetu wa kufua umeme wa Rufiji. Ni kweli kabisa kwamba mradi huu una umuhimu mkubwa sana katika uchumi wetu, lakini hatua tuliyofikia ni point of no return.

Mheshimiwa Spika, hofu ambayo imejengwa ni juu ya vyanzo vya maji, na mimi niseme tu nimefanya ziara katika Mikoa sita ambayo inapatikana mito mikuu mitatu inayolisha Bonde la Mto Rufiji. Mto Luwengu ambao unachangia zaidi ya asilimia 19, Mto Ruaha Mkuu unachangia asilimia 15.5 na Mto Kilombero ambao unachangia asilimia 65.5. Vyanzo vya maji vya mito yote hii mitatu viko salama. Ningeomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge na Watanzania kwamba maeneo yote ambayo mito hii imeanzia vyanzo viko salama. Kazi tuliyonayo sasa ni ku-maintain vile vyanzo vya maji, lakini maji yanakopita mpaka kwenda kwenye Bonde la Mto Rufiji ndiko kazi tunayoifanya kuanzia sasa. Kwa hiyo nimefika mpaka Stiegler’s Gorge kwenyewe kwa kweli maji yapo ya kutosha na mradi huu utakuwa ni mradi wa mfano na utakuwa ni mradi endelevu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala la mazingira Serikali imeweka utaratibu mzuri sana. Vile viumbe hai tunavi-reserve; tukishamaliza mchakato mzima wa lile bwawa maana yake viumbe hai vile vinarudishwa na shughuli inaendelea kama ilivyo. Vilevile bado pale kutakuwa na faidi nyingi, wameeleza Waheshimiwa Wabunge vizuri; utalii, kilimo na vitu vingine vyote.

Mheshimiwa Spika, pia imezungumzwa tutavunja mkataba wa World Heritage, kitu ambacho siyo kweli. Mkataba huu wa World Heritage umekuja baada ya program hii kuanza, sasa program hii ikishaanza Selou kuwa World Heritage maana yake ule mkataba unakubaliana na program iliyokuwepo. Kwa hiyo nisingependa jambo hili lizungumzwe kwa kupotosha Bunge hili; kwamba tayari mkataba huu umekuja wakati program yetu ya Stiegler’s Gorge ilishakuwepo before. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunaandaa master plan kwa ajili ya ku-maintain vile vyanzo vya maji kama Wizara ya Mazingira na sisi tayari tumefungua ama tumeshaweka Ofisi ya Baraza la NEMC pale pale. Yuko mratibu ambaye atakuwa anashughulika na mazingira, pale pale kwenye eneo la Stiegler’s Gorge. Kwa hiyo nilitaka niwaondoe hofu Waheshimiwa Wabunge kwamba suala hili la mradi huu …..

T A A R I F A

SPIKA: Kwa nusu dakika, Mheshimiwa Msigwa.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, yeah, nilitaka nimwambie rafiki yangu nimpe taarifa kwamba Selous kuwa ni World Heritage si leo, hata Bunge lililopita Serikali ilipotaka kuchimba Uranium ilitutuma baadhi ya wajumbe kwenda Urusi kuomba UNESCO itoe kibali tuchimbe Uranium.

Sasa ukisema Selous hiyo World Heritage imeanza leo, nilikuwa nakupa taarifa kwamba tulianza muda mrefu, huu mradi wetu umeikuta Selous tuko World Heritage tayari. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri malizia dakika moja.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, nimsaidie kaka yangu Mheshimiwa Msingwa, nimefika Iringa bahati mbaya hukuwepo lakini ningeweza kukupa elimu zaidi, mradi umeanza tangu Nyerere kaka, si Bunge lililopita. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niendelee, nilitaka nimsaidie kwenye hili. Unapokuwa na umeme wa kutosha sisi watu ambao tuna-deal na eneo hili la mazingira ni msaada mkubwa sana, huwezi kuzungumzia asilimia tatu ya Selous. Watu wanapopata umeme leo wamesema Waheshimiwa Wabunge, sasa tutaacha kutumia kuni, mkaa na vitu vingine vyote, watu wata-transform kutoka kwenye matumizi haya wanaanza kutumia umeme. Nilitaka niwaondoe hofu mradi huu tunauhitaji sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)