Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Ester Alexander Mahawe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. ESTER A. MAHAWE: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nitoe pongezi za dhati kwa Wizara ya Nishati, nikianza na Mheshimiwa Waziri Kalemani, Naibu Waziri Subira Mgalu pamoja na Watendaji wote wa Wizara wakiongozwa na Katibu Mkuu. Kazi kubwa imefanyika katika awamu hii ya tano chini ya Serikali makini inayoongozwa na Jemedari wetu Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli ya kuhakikisha vijiji, vitongoji na kaya zote zinapata umeme ifikapo mwaka 2025.

Mheshimiwa Spika, hivi sasa mradi wa REA III tayari umepeleka umeme katika maeneo yote ya liyopitiwa na msongo wa umeme wa Kilovoti 400 yenye urefu wa kilomita 670. Kero ilikuwa kubwa, hata hivyo ni imani yangu kwa sasa wananchi hawa watajenga imani kubwa kwa Serikali yao makini. Pamoja na kazi nzuri inayofanywa ya kuzima vibatari vyote katika kaya zote ifikapo 2025, bado kuna vijiji vingi sana havijapatiwa umeme katika Mkoa wa Manyara. Niiombe Wizara kupitia kwa Mheshimiwa Waziri kuuangalia mkoa huu kwa jicho la huruma kwani mpaka sasa vijiji vilivypata umeme ni vichache kuliko ambavyo bado havijapata umeme.

Mheshimiwa Spika, changamoto hiyo ya mkoa wetu hasa vijiji vyake ni kwamba kutokuwekeza umeme kunaziathiri zaidi taasisi mbalimbali za kijamii kama vile shule za sekondari, zahanati pamoja na vituo vya afya. Jambo hili linalorudisha nyuma maendeleo ya wananchi wetu na hata wengine kutopata huduma stahiki hasa ya kitabibu.

Mheshimiwa Spika, kwa ufupi sana naomba nigusie suala la deni kubwa la TANESCO. Deni hili limekuwa kubwa sana kwa kuwa linachagizwa na gharama ya upelekaji wa miundombinu ya gesi kutoka Mtwara. TANESCO ndiyo wanaoligharimia bomba hilo la gesi, jambo ambalo linafanya gesi hiyo kuwa ghali na umeme kuuzwa kwa bei kubwa sana. Umeme wa TANESCO utauzwa kwa bei nafuu pale tu ambapo Serikali itaipunguzia TANESCO gharama ya miundombinu ya gesi bomba.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja na naomba kuwasilisha.