Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia 100.

Mheshimiwa Spika, Wizara hii chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Medard Matogolo Chananja Kalemani, imetutendea makuu. Miradi ya REA III na Makambako – Songea 220kv grid imetutoa matongotongo sisi Wana- Namtumbo. Katika mwaka huu wa fedha wa 2018/2019 Namtumbo imenufaika kwa baadhi ya vijiji vyake kuwashiwa umeme. Nikuombe Mheshimiwa Waziri tufikishie shukrani zetu sisi Wana-Namtumbo kwa Kiongozi Mkuu, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha zilizowezesha mtukune sisi Wana-Namtumbo katika sekta hii ndogo ya umeme. Hakika tumepata kiongozi anayetujali hata sisi wakazi wa Wilaya ya Namtumbo.

Mheshimiwa Spika, naamini Mheshimiwa Waziri atatekeleza kauli yake aliyoitoa Namtumbo tarehe 05/04/ 2019 mbele ya Mheshimiwa Rais kuwa vijiji vyote na vitongoji vyote vya Wilaya ya Namtumbo vitafikishiwa umeme. Katika kulitekeleza hili, nikuombe uwakumbushe REA kusaini addendum inayompa ridhaa na nguvu mkandarasi wa REA III wa Namtumbo kusambaza umeme kwenye vijiji vyote vilivyobaki, hususan vijiji vya Kata za Limamu, Ligera, Lisimonji, Lusewa, Msisima na Magazini. Maeneo hayo ndiyo yanayotarajiwa kuunda Wilaya ya Sasawala ambapo Lusewa ndiyo makao makuu. Lusewa kwa sasa ni mamlaka ya mji mdogo na hivyo ni muhimu sana kutufikishia umeme wa uhakika kutokana na uchumi wa eneo hilo. Hongera sana wewe, Naibu wako na watendaji wote wanaokusaidia.