Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Sonia Jumaa Magogo

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. SONIA J. MAGOGO: Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kwa kuipongeza Wizara kwa jitihada kubwa wanazofanya pamoja na kwamba bado kuna baadhi ya changamoto zinazotakiwa kufanyiwa kazi.

Mheshimiwa Spika, kuna baadhi ya vijiji katika Mkoa wa Tanga bado havijafikiwa na mradi wa REA. Pamoja na kwamba jitihada za Wizara tunaziona lakini tunaomba kasi zaidi ili vijiji vilivyobaki vipate umeme.

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Bomba la Gesi la Hoima ulenge zaidi kuwanufaisha wananchi wazawa wa maeneo husika kwa kuwapa elimu ya kutosha juu ya opportunities zilizopo na ni jinsi gani wanaweza kuzifikia. Pia, ikibidi wasaidiwe mitaji au mikopo maana kwa kufanya hivi wananchi hawa ndio watakuwa walinzi wa kwanza wa miundombinu ya mradi huu.

Mheshimiwa Spika, la mwisho, niiombe Wizara itoe elimu ya kutosha juu ya matumizi ya gesi asilia majumbani na viwandani na kuongeza kasi ili ienee kwa watu wengi zaidi, maana manufaa yake ni mengi na ni makubwa kwa ustawi wa nchi yetu kiuchumi na hata katika utunzaji wa mazingira.

Mheshimiwa Spika, kwa kumalizia niiombe Wizara iangalie maeneo ambayo miradi hii inatekelezwa; kwa mfano Kinyerezi. Jamii inayozunguka miradi hii ipate faida na kufikiriwa kwa mfumo wa give back to the society. Unakuta miundombinu; mfano ni eneo lililopo mradi wa Kinyerezi, barabara ya kuendea katika mradi huu ni mbovu sana na magari yenye mizigo mizito yanaenda katika mradi yakichangia, hivyo kuwapa hali ngumu sana wananchi wa eneo hilo.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.