Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Spika, nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri Dkt. Kalemani na Naibu Waziri Mheshimiwa Mgalu, wanafanya kazi nzuri sana.

Mheshimiwa Spika, naomba kuchangia kuhusu mradi wa REA. Liko tatizo eneo langu la Tabora Kaskazini. Mkandarasi hafanyi vizuri, kasi yake ni ndogo sana. Niliomba kipaumbele eneo la vijiji anavyotoka Mbunge ambako kuna vijii barabarani; Vijiji vya Kasenga, Majengo, Kanyenye, Ikongolo, Nzubuka na Izugawima. Vijiji hivi vyote viko barabarani na ndiko Mbunge anakotoka.

Mheshimiwa Spika, naomba Mheshimiwa Waziri rafiki yangu, ndugu yangu niletee umeme katika vijiji hivyo ni muhimu sana. Kuna shule za msingi tano na shule za secondari mbili na zahanati pekee katika kata hiyo ya Ikongolo. Nakushukuru sana sana Mheshimiwa Waziri tafadhali sana; vijiji vya Kasenga, Majengo, Ikongolo, Kanyenye na Nzubuka ni muhimu sana. nakuomba Mheshimiwa Waziri Kalemani. Natanguliza shukrani.