Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Maria Ndilla Kangoye

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. MARIA N. KANGOYE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia fursa ya kuchangia hotuba ya Waziri wa Nishati kwa njia ya maandishi. Nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Kalemani, Waziri wa Nishati pamoja na Naibu Waziri wake Mheshimiwa Subira Mgalu kwa kazi nzuri wanayofanya ya kusimamia shughuli nzima ya usambazaji wa umeme katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, pamoja na umakini wa Wizara katika usambazaji wa umeme bado kumekuwa na changamoto ya wakandarasi wa kutekeleza miradi ambapo huchukua muda mrefu tofauti na mikataba inavyotaka. Nazidi kuwapongeza Waziri na Naibu wake kwa kusimamia umeme wa REA. Ombi langu ni kwamba wazidi kusisitiza vituo vya afya na shule yote ili kuweza kurahisisha huduma husika.

Mheshimiwa Spika, kabla sijahitimisha mchango wangu, naomba nimkumbushe Mheshimiwa Waziri kwamba, aliwahi kuahidi umeme wa uhakika Kata ya Kibakwe, Wilaya ya Magu na bado wananchi tunakumbuka ahadi hiyo na tuna matumaini makubwa juu ya utekelezaji wake.

Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi ya kuchangia, naunga mkono hoja kwa asilimia mia.