Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. John John Mnyika

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kibamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Spika, mradi wa umeme Kinyerezi, Dar es Salaam- Arusha kupitia Kibaha- Chalinze, wakazi wa Kata ya Kinyerezi kwenye mitaa ya Kiboga na Kifuru walifanyiwa tathmini kwa ajili ya kupisha mradi wa njia ya umeme tangu mwezi Septemba, 2016, lakini mpaka sasa mwaka wa tatu wamesimamisha shughuli za maendeleo na Serikali hawaelezi chochote. Katika majumuisho yake Mheshimiwa Wizara ieleze ni lini hasa wananchi hao watalipwa fidia?

Mheshimiwa Spika, pia Wizara ieleze katika Kata za Jimbo la Kibamba za Kwambe, Mbezi, Msigani, Goba, Saranga na Kibamba yapo maeneo mpaka sasa umeme haujafika. Ni lini TANESCO itahakikisha maeneo yote yanafikishiwa umeme? Katika kata hizo kuna kawaida pia ya umeme kukatikakatika na kupungua nguvu (low voltage). Serikali katika swali langu Bungeni iliahidi ufumbuzi lakini mpaka sasa tatizo hilo limeendelea.