Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Spika, Kuhusu Umeme wa REA. Tumeshuhudia Mawaziri wakizindua umeme kwenye nyumba za tembe, nyumba za nyasi, nyumba ambazo kwa upepo kidogo tu zitaanguka. Hivi kuna haja gani kuweka umeme ambao siku nyumba zikianguka mnaweza kusababisha madhara? Tumeshuhudia mijini tu shoti ya umeme nyumba zinaungua na kuteketea. Kwanini Wizara isingeshirikiana na TASAF kwanza zikaboreshwa nyumba za Watanzania (kaya) maskini kabla ya umeme?

Mheshimiwa Spika, umeme REA Phase ll. Katika Manispaa ya Morogoro Kata ya Mindu inapitiwa na umeme wa grid ya taifa lakini wananchi wake hawana umeme katika baadhi ya maeneo. Mheshimiwa Naibu Waziri alikuja Morogoro na wananchi walitoa malalamiko hayo; kwanini mpaka sasa wananchi hawapati umeme?

Mheshimiwa Spika, Kuhusu Stieglers George Project. Watanzania wanapaswa kuona mkataba huo. Tafiti zilizofanywa na World Energy Resource zinaonesha kuwa project hiyo itatumia fedha nyingi zaidi ya kiwango kinachotarajiwa. Ni vyema Watanzania tukawekwa wazi.

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Kidunda Morogoro uliokuwa na mpango wa uzalisha umeme MW 20, ulikuwa na mkakati wa kuendeleza kilimo, kutoa maji kwa wakazi wa Dar es Salaam, Pwani, Tanga na kadhalika. Kuna haja gani Serikali kuanzisha project hazi-take off mna-jump kwenye new project? Kidunda bado tupo Stiegler’s, gesi bado tumekimbilia Stieglers?