Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, kwanza naunga mkono hoja hii iliyo mbele yetu. Nampongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa kazi nzuri sana na kwa wanavyojitoa katika kuwatumikia Watanzania na kuhakikisha kuwa Watanzania wanapata umeme vijijini kwa maendeleo yao; lakini pia kwa kutekelea Ilani ya Uchaguzi ya CCM.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri, mkandarasi wetu Wilaya ya Nyang’hwale kasi yake sio nzuri sana ya kusambaza umeme. Sababu anazozitoa anadai kwamba yeye amekwamishwa na upungufu wa nyaya.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu kwa Mheshimiwa Waziri, ili kuhakikisha usambazaji huu wa umeme kwa Wilaya ya Nyang’hwale tutatulieni tatizo hilo la nyaya kwa wakandarasi wako. Ukizingatia tunaenda kwenye uchaguzi wa Serikali za Mtaa na Uchaguzi Mkuu 2020.

Mheshimiwa Spika, pale Makao Makuu ya Wilaya ya Nyang’hwale, yaani Khalumwa tayari umeme upo ila baadhi ya maeneo mengi ya Mji wa Khalumwa hayana umeme na sababu kuu ni upungufu wa nguzo na nyaya. Mheshimiwa Waziri nakuomba sana tutatulie mapungufu hayo, wananchi wako tayari kufunga umeme.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.