Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Ester Michael Mmasi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. ESTER M. MMASI: Mheshimiwa Spika, ushauri wangu kwa Serikali, napendekeza Wizara ione umuhimu wa kuleta Sheria ya Mafuta Namba 21 ya Mwaka 2015 Bungeni ili Bunge liweze kufanya marekebisho ya sheria hii. Ni rai yangu Serikali iweze kurejesha mamlaka ya Waziri katika kutoa leseni za vitalu, lakini pia, vibali vya uchimbaji wa gas & oil. Ni ushauri wangu Serikali iweze kuondoa sharti la sheria la asilimia 3 kwenye Mfuko wa Rasilimali ya Gesi na Mafuta ili kuruhusu matumizi ya Mfuko wa Rasilimali ya Gesi na Mafuta kwenye miradi ya maendeleo. Mathalani shughuli za usambazaji wa gesi majumbani.

Mheshimiwa Spika, ni ushauri wangu kwa Wizara ya Fedha kuona umuhimu wa kutoa fedha yote kama ilivyoombwa na Taasisi ya TPDC juu ya uanzishwaji wa Kituo cha CNG (ie, Compressed Natural Gas) Mlalakuwa, Ubungo. Taasisi hiyo kupitia Wizara ya Nishati imeomba kiasi cha takribani TShs. bilioni 16; hapa ninapochangia mabasi ya UDART, yaani mabasi ya mwendokasi 300 yatakayoingia Tanzania Mwaka wa Fedha 2019/2020 yote yatatumia CNG. Mbali na hapo, tayari TPDC imeshapokea maombi ya wateja wakubwa wanne, wawili Kigamboni, wawili Kibaha, Pwani. Ninaona tuna sababu ya msingi ya kuhakikisha PST kupitia Wizara ya Fedha inatoa fedha zote kama ilivyoombwa na Taasisi ya TPDC.

Mheshimiwa Spika, pia ninashauri Serikali i-support pendekezo pamoja na kiasi cha fedha kilichoombwa na Wizara katika ukarabati wa Tank Number 8 la kuhifadhi oil & gas, yaani Strategic Oil & Gas Reserve Tanks, kwani kwa kufanya hivi Wizara itaondokana na adha ya ukodishaji wa maghala ya kuhifadhi mafuta na gesi. Tanzania leo hii ina reserve ya gesi kiasi cha futi za ujazo trilioni 57.54, lakini pia, Tanzania ina lita za petroli milioni 125.22, dizeli lita milioni 94.78 pamoja na mafuta ya taa na ya ndege lita milioni 18.34. Hivyo ninaona umuhimu mkubwa wa Wizara ya Fedha kuona umuhimu wa kutoa fedha zote za ujenzi na ukarabati wa Tank Number Eight kama ilivyoombwa na TPDC.

Mheshimiwa Spika, ikumbukwe nchi ya Japan ambayo haina gesi ardhini ina reserve kubwa ya gas & oil, na hata Trinidad; zote hizi zina reserve kubwa ya gesi kwa sababu walikubali kwanza kuwekeza kwenye miundombinu ya kuhifadhi oil & gas.

Mheshimiwa Spika, na mwisho, NAT Oil ambayo ni Taasisi ya Serikali kwenye biashara ya gesi na mafuta; ninashauri kwa moyo dhati Sheria ya Petroli iletwe Bungeni, ili TPDC iweze kushindana na kampuni za kigeni, kwa mfano Trafigura Oil & Gas Company from Singapore, Kampuni ya Addax, kampuni ya Uswizi iliyowekeza kwenye tasnia ya gesi na mafuta ambayo pia ndiyo kampuni ya Oryx. Vilevile hata Kampuni ya TOTSA from France yenye umiliki wa Total pamoja na Sahara from Nigeria.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha. Ahsante.