Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, pongezi kubwa kwako Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Mkurugenzi wa REA na TANESCO. Umeme utekelezaji unaendelea, lakini nguzo hakuna na waya. Nimeenda juzi nyumbani mafundi wanakaa wanangoja vifaa. Hata hivyo, nashukuru kwa kuongeza scope, asanteni, ila hiyo ndiyo inayoshusha performance ya utekelezaji wa Ilani.

Mheshimiwa Spika, TANESCO haina hasara kamili kutokana na kulazimika kama shirika la nchi kupeleka umeme hata maeneo yasiyolipa kwa sasa kama kichocheo cha uchumi na si tu kibiashara. Serikali inatimiza jukumu hilo kupitia Shirika lake la TANESCO.

Mheshimiwa Spika, hongereni kwa Stiglers na pia, kuwapa gesi Dangote. Viwanda oyee!