Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. ZAINAB M. AMIR: Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kuwapongeza Waziri wa Nishati pamoja na Naibu Waziri kwa kazi kubwa wanayoifanya katika Wizara hii ya Nishati katika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo. Naishauri Serikali kuwa fedha zinazotengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo zitolewe kwa wakati ili Wizara iweze kutekeleza majukumu yao kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, pia naishauri Serikali ianze kutumia nguzo za zege katika usambazaji wa umeme mijini na vijijini maana ni madhubuti na pia tutaepuka na uharibifu wa mazingira kwa kukata miti hovyo kwa ajili ya kupata nguzo za miti.

Mheshimiwa Spika, tatu naishauri Serikali ipunguze gharama ya uunganishaji wa umeme hususan maeneo ya mijini maana ni ghali sana. Ikipunguzwa wananachi watakuwa na uwezo wa kugharamia na kupata umeme maeneo mengi ya nchi yetu. Kuna vijiji vimepitiwa na nguzo za umeme jirani kabisa lakini hadi sasa vijiji hivyo havina umeme. Serikali ione sasa haja ya kuvipatia vijiji hivyo umeme wa uhakika.

Mheshimiwa Spika, nne bei ya umeme hususan mijini kwa matumizi ya majumbani kwa unit ni ghali mno. Naishauri serikali hii ya wanyonge angalau ipunguze bei ya umeme kwa unit maana ni kubwa sana. Pia naishauri Serikali kuhusu PINOT Project ya usambazaji gesi majumbani kwa bei nafuu, iliyofanywa maeneo ya Mikocheni Jijini Dar es Salaam. Huduma hii isambazwe katika maeneo mengi ili iweze kuwafikia wananchi wenye kipato cha chini.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali ianzishe kozi katika vyuo vyetu vikuu hapa nchini kwetu vya kudahili wanafunzi kusomea masuala ya gesi ili tuweze kuwa na wataalam wa kutosha kutoka hapa hapa nchini. Pia gharama za kusoma kozi ya gesi nje ya nchi, kwa mfano Uturuki, China na kadhalika ni gharama kubwa sana. Hivyo kozi hii ikianzishwa katika vyuo vyetu wanafunzi watapata fursa ya kusoma kwa urahisi.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali iajiri watendaji wa watumishi wa kutosha katika Wizara wengi wamekaririshwa na hawawezi kutoa maamuzi katika maumbo mbalimbali wakati wa kutekeleza majukumu yao.

Mheshimiwa Spika, mwisho nawaombea afya njema na umri mrefu Mheshimiwa Waziri wa Nishati pamoja na Naibu wake ili waweze kutekeleza majukumu yao ya kuwatumikia Watanzania katika kusimamia miradi mbalimbali ya maendeleo nchini mwetu.