Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Mahmoud Hassan Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA: Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Waziri Dkt. Kalemani na Mheshimiwa Naibu Waziri Subira Mgalu kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kuhakikisha wananchi wanapata umeme.

Mheshimiwa Spika, mchango wangu utajikita katika maeneo mawili. Kwanza maeneo ambayo hayana umeme. Katika Jimbo la Mufindi Kaskazini Kata ya Mpangatazara yenye Vijiji vya Mpangatazara na Kimbwe hakuna umeme kabisa. Pia katika Kata ya Ikwila hakuna umeme Kijiji cha Ikwila, Ilangamoto, Ugunza Kata ya Igombavanu, Vijiji vya Uhembila na Matikitu Kata ya Sadani Vijiji vya Ufosi na Mbugi, Kata ya Kobanga Kijiji cha Kipanga Kata ya Mdabulo Kijiji cha Ilasa, Kata ya Mapanda kijiji cha Chozo, Uhafiwa Ihimbo.

Mheshimiwa Spika, eneo la pili ni kuhusu mahusiano yetu ya wananchi wa Tarafa ya Kibengu na TANESCO. Mara ya mwisho mimi pamoja na Mheshimiwa Diwani wa Mapanda pamoja na Wenyeviti wa Vijiji wa Kata ya Mapanda pamoja na TANESCO tulifanya kikao kwenye ofisi ya Mheshimiwa Waziri Dkt. Kalemani na TANESCO waliahidi kuboresha miundombinu kwenye Barabara ya Uhemi, Uhafiwa mpaka Ihimbo; na barua waliniandikia mimi Mbunge kama mwakilishi wa wananchi. Hata hivyo, kwa masikitiko makubwa tunaenda mwaka wa pili hata kilometa moja hawajatengeneza.

Mheshimiwa Spika, namuomba sana Mheshimiwa Waziri aingilie kati. Juzi nilikutana na DG wa TANESCO naye aliahidi kama mwanzo.

Mheshimiwa Spika, jambo la mwisho ni gharama kubwa ya kuingiza umeme wa bwawa la Mwenga lililopo Wilaya ya Mufindi. Gharama zimekuwa kubwa sana kuliko zilizoelekezwa na Serikali, pia wana tabia ya kuwatishia watu. Naomba sana Mheshimiwa Waziri aje katika jimbo langu kama alivyoahidi ili aone hali halisi na matatizo wanayoyapata wananchi kutokana na ukiritimba na wawekezaji wa Mwenga Hydroelectric power.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.