Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Spika, natoa mchango kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, REA awamu ya III ilipanga kupeleka umeme Wilaya ya Nkasi vijiji 51. Wilaya yenye Majimbo mawili ya uchaguzi lakini Jimbo langu lilipata vijiji 12 tu; pamoja na maombi ya nyongeza nimekuwa napewa maneno ya faraja bila utekelezaji wowote.

Mheshimiwa Spika, Mawaziri na wataalam lazima wajue sikujileta hapa, nililetwa na wananchi lazima wagawe resources za nchi kwa usawa. Mara zote nikionesha maombi ya kunisaidia napewa maneno ya kufariji tu, hakuna hata kijiji kimoja kilichoongezwa katika vijiji 15 nilivyoomba vya nyongeza. Naomba Waheshimiwa Mawaziri wangu nawapenda sana na nimeisemea hapa Bungeni Wizara nikiwa Mjumbe wa Kamati.

Mheshimiwa Spika, hadi sasa wanipe Vijiji vya Katani, Malongwe, Wampembe, Izinga, Ng’undwe, Sintali, Nkana, Mkomanchindo, King’ombe, Mlambo, Kilambo, Mpasa, Tundu, Lolesha, Kala, Mwinza, Lyapinda, Lupata, Msamba, Kisambara, Ninde na Nakasanga ili kuleta usawa.