Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, kuchelewa kukamilika miradi ya umeme jua katika Visiwa vya Ukerewe; mradi wa usambazaji umeme kwenye visiwa mbalimbali vya Ukerewe unaendelea kwa kusuasua sana. Mfano, Kisiwa cha Ukara (JUMEME), mradi umesimama kwa muda mrefu kwa sababu mbalimbali hali inayokatisha tamaa wananchi waliokuwa wanasubiri kwa hamu. Ushauri wangu, Wizara itie msukumo ili miradi hii ikamilike kwa haraka.

Mheshimiwa Spika, bei ya umeme unaozalishwa na JUMEME kuwa na bei kubwa mno; bei ya umeme unaozalishwa na JUMEME ni kubwa sana kiasi ambacho kinakatisha tamaa wananchi kuutumia umeme huo. Mfano, unit moja katika Kisiwa cha Ukara (Eneo la Bwisya) ambapo tayari wameanza kutumia huduma hiyo ni Sh.3,000. Bei hii ni kubwa sana kiasi ambacho wananchi wanashindwa kumudu na kusitisha huduma.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa jambo hili tayari limeongelewa na kuachiwa EWURA kutoa maelekezo, basi naomba Wizara iweze kufuatilia kwa karibu na kuisukuma EWURA iweze kutoa maelekezo ili wananchi wanaotumia umeme huu wafarijike na kuongeza watumiaji jambo litakalotia moyo wawekezaji hawa vilevile.

Mheshimiwa Spika, kukatikakatika kwa umeme kwenye eneo la Ukerewe; kumekuwa na tatizo la kukatikakatika kwa umeme kwenye Visiwa vya Ukerewe. Maelezo yanayotolewa ni kuanguka kwa nguzo kila mvua ikinyesha, hali hii inaathiri sana uchumi wa visiwa vya Ukerewe. Ushauri wangu, itafutwe suluhu ya kudumu ya tatizo hili ili tatizo hili la kukatika mara kwa mara kwa umeme liishe na kuwaondolea hasara wananchi wa Ukerewe wanaoshughulika na shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Mheshimiwa Spika, kusuasua kwa Mradi wa REA. Pamoja na jitihada kubwa za Wizara, bado vijiji vingi na vitongoji havijaweza kupata umeme na hata maeneo yaliyofikiwa na umeme, wigo wa watu wanaopewa umeme huo umekuwa mdogo sana na hivyo tija kutoonekana. Mfano, katika kijiji chenye kaya zaidi ya 300 unapopeleka umeme kwenye kaya 10 tu ni tatizo kubwa.

Mheshimiwa Spika, lakini pia mradi wa ujazilizi uende kwa haraka hasa Wilayani Ukerewe ili kuondoa tatizo la nishati ya umeme kwenye maeneo yaliyorukwa.