Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Spika, pongezi nyingi kwa Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri wa Nishati, Katibu Mkuu na Wakuu wa Idara zote kwa kazi kubwa wanazofanya za kusambaza umeme nchini, Urambo ikiwemo, tunashukuru sana. Naomba jitihada za kujenga kituo cha kupoza umeme Urambo ziendelee, nawatakia kila la heri.

Mheshimiwa Spika, naomba maeneo yafuatayo yapate umeme. Orodha ya awali imeletwa Wizarani. Kata Kapilula eneo la Ulasa B, Kata ya Urambo, eneo la Ubalani, Mabatini, Boma Village, Kata ya Kiyungi eneo la Tulieni na Kata ya Imalamakoye eneo la Imalamakoye D. Taasisi- Magereza Urambo - pump ya maji, Shule ya St. Lucia - Kata ya Ukondamoyo na Shule ya Magole - Kata ya Vumilia. Tunaomba umeme wa REA ufike vijiji vyote vilivyobaki.