Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. ENG. RAMO M. MAKANI: Mheshimiwa Spika, pongezi; hongera sana kwa Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu, Wakurugenzi, Wataalam wote, Wakuu wa Taasisi hususan REA na Watumishi wote wa Wizara.

Mheshimiwa Spika, kazi ya kutekeleza malengo kama yalivyoanishwa katika Ibara ya 43(c), 43(f) na 43(g) kwa mfano, Ilani ya CCM imetekelezwa na inaendelea kutekelezwa kwa kiwango kikubwa. Hongera kwa Wizara, Serikali kwa upana wake chini ya Mheshimiwa Dkt. Magufuli, Rais wa Awamu ya Tano, hongera sana kwa CCM. Tukiendelea hivi na pengine kuongeza kidogo kasi na ufanisi, sekta ya nishati inakwenda kupaisha nchi.

Mheshimiwa Spika, hali ya usambazaji umeme chini ya REA; Jimbo la Tunduru Kaskazini; Mheshimiwa Waziri kwanza nashukuru kwa kazi kubwa iliyofanyika Tunduru Kaskazini, hata hivyo nimeambatisha hapa orodha ya vijiji ambavyo bado vinahitaji kuwekewa msukumo ili navyo vinufaike na maelekezo ya Ilani ya CCM.

Mheshimiwa Spika, upatikanaji wa umeme Tunduru; Mheshimiwa Waziri kwa miaka mingi tangu tupate uhuru hali ya upatikanaji umeme Tunduru ilikuwa duni sana. Tunashukuru kwa kutuunganisha katika gridi ya Taifa kupitia Mahumbika- Lindi-Mtwara circuit. Pamoja na mafanikio haya tunaomba umeme wa gridi ya Taifa kutokea Route ya Makambako. Songea-Namtumbo usiishie Namtumbo bali uendelezwe hadi kufikia Tunduru ili upatikanaji wa umeme Tunduru uwe wa kutosha na kuaminika zaidi.

Mheshimiwa Spika, ifuatayo ni orodha ya vijiji visivyokuwa na umeme Tunduru-Kaskazini katika Hamashauri ya Wilaya ya Tunduru.
N a . K A T A V IJI JI V IT O NG O J I V IK U B W A
1 . J a kika K in d a m b a Ja r ib u n i
2 . K id o d o m a L e g e z a m w e n d o M a c h e m b a
M a ji y a S w e la
3. L ig un g a T w e n d e m b e le M b a r ik iw a
4 . N a k a p a n y a T u lie n i M c h o lo l o
5. N a m iu n g o N a m m a n g a Na n g o lo m b e
M n e n je
Pa c h a n n e
M ta n d ik a
6. M a jim a ji M g et a
So n g a m b e le
7. N a m w in yu C h a n g a r w a w e B
8 . S is i k w a S is i L e lo le lo Se v u y a n k e Na k a te te
9 . M a so n y a N a m b a r a p i
M k a le k a w a n a
10 . M L. M a g ha r ib i M k o n d a M a lo m b e
M s in jili
11 . N g ap a N g a p a
M n a z im m o ja C h a w is i N g a p a M t o n i Jiu n g e n i
12 . M u h u w e s i T e m e k e
M w a n g a z a
13 . M in d u L iw a n g ula
1 4 . N a m a k a m b a le R w a n d a
15 . M a te m a n g a Fu n d i m b a n g a
1 6 . M c h a n g a n i M c h a n g a n i Ng a lin je
K id u g a lo
1 7 . N a n d e m b o T u m a in i Am k a
Na n g u n g u lu
1 8 . K a lu lu R a h a le o
M b u n g u la ji
Ju m la 3 0 (2 7 ) 1 4

Mheshimiwa Spika, vijiji vya Kata tano za Tinginya, Nakayaya, Mlingoto Mashariki, Nanjoka na Majengo vina umeme na kimoja kilichobaki kwa Kata ya Nampungu kiko kwenye mpango wa phase III, round I.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vitongoji vilivyoorodheshwa ni vikubwa na vinajitegemea na vina shughuli nyingi na watu wengi.

Mheshimiwa Spika, Vijiji vya Nangungulu na Amka viko jirani na Nandembo lakini vinajitegemea, pia Kijiji cha Mchangani ni kikubwa sana na kina eneo muhimu lisilokuwa na umeme.