Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu kuwawezesha Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Watumishi wote kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kujituma na kujitoa kwa maslahi ya maendeleo ya kuwasambazia umeme wananchi hadi vijijini na vitongoji vyote nchini hadi sasa wana asilimia ya kuridhisha na matumaini ya kutimiza azma ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ya ahadi ifikapo mwaka 2025 umeme uwafikie wananchi wake.

Mheshimiwa Spika, napenda kutoa shukurani za dhati kwa Meneja wetu wa TANESCO, Ndugu Chambua kwa kazi nzuri anayoifanya pamoja na changamoto zilizopo ndani ya Mkoa wa Rukwa.

(1) Wakandarasi hawajapatiwa nyongeza ya vifaa vya kupeleka umeme kwenye Taasisi za Serikali (zahanati, vituo vya afya, shule za msingi na sekondari zetu).

(2) Nguzo zilizosambazwa zisiwe picha kwa wananchi, ni vyema zikakamilishiwa zoezi na umeme kupatikana

Mheshimiwa Spika, pamoja na shughuli na jitihada za Waziri na Naibu Waziri kwa moyo wa dhati wa kuitumikia Wizara hii, bado Mkoa wa Rukwa tunahitaji umeme kwani kazi iliyofanyika bado vijijini Mwambao wa Ziwa Tanganyika, Ziwa Rukwa bonde zima, mpakani mwa Zambia na Congo DRC hali ni ngumu bado. Tunaomba umeme vijijini zaidi, tunashukuru hiyo jitihada ya kupatiwa umeme wa gridi ya Taifa kuingia Sumbawanga ni tija ya pekee kwetu.

Mheshimiwa Spika, tunaomba jitihada iongezeke kwa kusambaza umeme Mkoa wa Rukwa na kutuwezesha kwa kuongeza nguvu zaidi.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.