Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, napenda kuchangia hotuba hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mradi wa REA katika Jimbo la Tunduru Kusini kuna vijiji vitano tu kati ya vijiji 65, hivyo naomba vijiji vya nyongeza nilivyoomba viingizwe kwenye REA lll, awamu ya kwanza, Vijiji hivyo ni Semeni, Mtina, Angalia, Nasya, Tuwemacho, Chemchem, Ligoma, Mkoteni, Namasakata, Luwingu, Nalasi, Chilundundu, Lipepo, Mchoteka na kadhalika ili kupunguza idadi kubwa ya vijiji visivyokuwa na umeme.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo naomba Serikali inapopanga vijiji waangalie sana Halmashauri zenye majimbo zaidi ya moja kuchukua vijiji kila upande wa jimbo ili kupunguza malalamiko.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa umeme unawekwa kwenye vijiji vingi ni vizuri TANESCO wakafikiria ofisi ndogo katika tarafa ili kutoa huduma kwa haraka kwa wateja wake.

Mheshimiwa Spika, katika miradi ya REA kuna changamoto ya mafundi wanaoweka nyaya (wiring) kwenye nyumba za wananchi kuwa na gharama za juu kuliko uhalisia wa kazi, ni vizuri TANESCO wangetoa mwongozo kwa wakandarasi na mafundi wanaofanya wiring katika majumba ya wananchi juu ya bei na gharama za kufanya wiring.

Mheshimiwa Spika, viongozi/management ya TPDC wateuliwe viongozi wa kudumu badala ya kuwa na makaimu kila siku ambapo wanakosa ujasiri wa kutoa maamuzi kwa kuhofia vyeo vyao kuyeyuka na kwa kuwa mpango kazi uliopo unaonyesha matumaini ya Shirika/TPDC kukua ni vyema basi management ya kudumu ikawekwa badala ya kuweka makaimu katika kila idara ya TPDC.

Mheshimiwa Spika, gharama ya bomba la gesi ichukuliwe na Serikali badala ya kuwatwisha mizigo TPDC ili kupunguza bei ya gesi kama inavyolalamikiwa na wawekezaji wengi. Hii itasaidia kuvutia wawekezaji wengi zaidi kutumia gesi katika kuendesha viwanda vyao na kwa matumizi ya majumbani.

Mheshimiwa Spika, TPDC iharakishe usambazaji wa gesi majumbani ili kuongeza kiwango cha gesi kinachotumika na kuongeza pato la TPDC na Serikali kwa ujumla.