Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, napenda kuchangia Wizara hii ya Nishati ambayo ni Wizara muhimu katika maendeleo ya kiuchumi na kisiasa. Sasa nitashauri mambo kadhaa katika Wizara hizi.

Mheshimiwa Spika, soko huria kwenye usambazaji wa umeme; kumekuwa na malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa wananchi kuhusu usambazaji wa umeme ukiwa wa kusuasua, hivyo nashauri Serikali kukubali suala la soko huria ili kuleta ushindani na kuleta tija kwa wananchi.

Mheshimiwa Spika, umeme wa upepo; Serikali ina mkakati gani wa kuwekeza nguvu ya kipesa na kutoa kipaumbele kuwasaidia watumiaji wengi ambao wana hali ya chini ili waweze kutumia umeme ambao utakuwa wa bei nafuu na utawanufaisha wananchi walio wengi.

Mheshimiwa Spika, Wakala wa Umeme Vijijini; kumekuwa na malalamiko makubwa juu ya mgao wa umeme unavyotekelezwa kwa kuwa kuna kuruka baadhi ya vijiji aidha kwa makusudi au kwa bahati mbaya. Ni vyema suala hili likafuatiliwa kwa ukaribu na umakini mkubwa sana ili kuondoa malalamiko yanayowakabili wananchi wengi.

Mheshimiwa Spika, TANESCO wapewe ushindani; TANESCO wamekosa ufanisi kiutendaji kwa sasa wanafanya kazi kwa mazoea, ni vyema kuwe na makampuni ili kuleta matokeo chanya na kuleta ufanisi kwa utekelezaji wa ugawaji umeme na nidhamu kwa matumizi ya pesa.

Mheshimiwa Spika, suala la umeme jazilizi; kumekuwa na ubaguzi mkubwa na watu wengine kujiona wanyonge pale wanapoona wananchi wengine wanapata umeme huku wengine wakikosa wakati wako eneo moja. Pia maeneo ya taasisi yepewe kipaumbele.

Mheshimiwa Spika, wakandarasi walipwe kwa wakati; kumekuwa na changamoto kubwa katika utendaji pale ambapo inatokea mkandarasi hajapewa malipo yake inapelekea kazi na miradi mbalimbali kusimama na kupelekea wananchi kuinuka kiuchumi.

Mheshimiwa Spika, bei halisi ya kuunganisha umeme; kumekuwa na mkanganyiko wa bei halisi ya umeme kwa wananchi wanapokuwa wanatakiwa kuunganishiwa pale ambapo REA inaishia bei zao zimekuwa tofauti kwa wananchi. Nashauri Serikali kufuatilia jambo hili na kutoa ufafanuzi.

Mheshimiwa Spika, maeneo yaliyobakia katika Mkoa wa Rukwa; tunaomba kujua ni lini maeneo hayo yatapata umeme kwani maeneo hayo yaliyobaki yakipata umeme yatasaidia kupunguza vifo vya akinamama na mtoto pia itawasaidia watu kiuchumi katika viwanda na biashara ndogondogo.