Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Spika, kwanza nichukue nafasi hii kukushukuru kwa kunipa nafasi hii. Lakini nichukue nafasi hii vilevile kumpongeza Waziri na Naibu wake kwa kazi nzuri wanazofanya, kwa kweli mnaitendea haki Wizara hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, muda wangu mi mdogo tu, nazungumzia suala la LNG ambalo mazungumzo yanaonekana yanachukua muda mwingi. Mazungumzo kuchukua muda mwingi yawe productive, yawe na uangalifu wa kutazama maslahi mapana ya nchi. Na ecosystem sasa hivi imekuwa introduced ambayo badala ya kufanya LNG wanafanya FNG (Floating Natural Gas Products).

Mheshimiwa Spika, na huu ni mtambo ambao unafungwa baharini kulekule kwenye meli na meli inabeba mzigo mkubwa sana wa mtambo huu na gharama za kuzalisha na kusafirisha gesi inakuwa ni ndogo. Na results zake ambazo Serikali itazipata na nafasi ya kutengeneza mtambo huu ni miaka miwili tu, tofauti na miaka tisa ambayo LNG inafanya kuleta kwenye shore ya nchi kavu, kwa hiyo watu wanaona labda ni muda mwingi sana.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo ninaomba Serikali katika mazungumzo yao wa-incorporate na waone umuhimu wa ku-introduce FNG badala ya LNG. Najua FNG ni component moja, haitakuwa kwa mradi wote, lazima LNG iwepo, lakini tunaweza tukaanza na FNG ili Serikali ikaanza kuvuna mapato yake kwa haraka sana kwa gharama za FDI ambayo ni Foreign Drect Investment, bila Serikali kuweka hela zake. Na wana-estimate FNG kuweza kuiletea Serikali kwa kipindi cha miaka mitatu labda two billion US Dollars.

Mheshmiwa Spika, kitu muhimu kwenye mikataba lazima wataalam wetu wawe na uhakika wa outflow meter waweke digital wireless meters ambazo zina sensor na kuona gas inayotoka. Hata wewe ukiwa ofisini hapa unaweza ukaona sensors za outflow meter ya internet of things ambazo zitakuwa zinafanya kazi huko Lindi, wewe utaona kiasi gani cha gesi kinatoka na hakuna nchi wala hakuna mahali popote wawekezaji hawa wataweza kuiibia Serikali.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri, kwa hiyo, naomba katika mazungumzo mjaribu ku-introduce FNG ili tunaze na FNG Serikali ipate mapato. Na katika kuanza mradi huu Serikali ihakikishe inaweka digital wireless meters za kuweza ku-sense gesi itakayokuwa inauzwa nje ili tusiibiwe katika mapato ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, baada ya maneno hayo, naunga mkono hoja. (Makofi)