Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. GEORGE B. SIMBACHAWENE: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nichukue nafasi hii kukushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia katika Wizara hii ya Nishati.

Mheshimiwa Spika, nianze kwa kumpongeza sana Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watendaji wote wa Wizara hii kwa kazi nzuri wanayofanya na hasa ya kupeleka umeme vijijini, wanafanya kazi nzuri wanazunguka na kufanya kazi ambayo Taifa hili ipo siku litapiga hatua kubwa kwa sababu umeme ndiyo uchumi.

Mheshimiwa Spika, rai yangu kwenye eneo hili ni kwamba umeme huu utakuwa na maana kijamii na kiuchumi endapo utakwenda kwenye huduma za jamii; uende kwenye shule, zahanati, vituo vya afya, visima vya maji na sehemu za uzalishaji vijijini ndipo tutakapoona namna umeme huu unavyokuwa na maana kwa kupelekwa vijijini. Vinginevyo, kama si hivyo basi umeme huu utakuja kutafsiriwa baadaye kwamba ni kitu ambacho tumewekeza sana lakini hakijaleta tija katika uchumi lakini ikifika katika maeneo hayo utatusaidia sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilikuwa na hotuba yangu ambayo niliiandaa lakini hapa ninaihairisha kwa sababu nataka nijaribu kuchangia kwenye line ambayo mdogo wangu Mheshimiwa Silinde amechangia na natambua kwamba ni Mjumbe wa Kamati ya Bajeti na hivyo ana ufahamu mkubwa na anayajua mambo mengi na tunashirikiana katika mambo mengi na sina mashaka hata kidogo juu ya uwezo wake, lakini nilitaka tu nimuongezee ujuzi juu ya masuala ya uchumi wa umeme. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Sera ya Dunia kwa sasa katika masuala ya umeme ni energy mixing, kwa nini? Energy mixing kwa sababu hakuna chanzo sustainable kwa sasa, iwe gesi inaisha; hiyo gesi unayosema inaisha, yawe maji yameathiriwa na uharibifu wa mazingira na yenyewe yanaisha, upepo mara utakuwepo mara hautakuwepo, chochote kile sasa hakina sustainability na ndiyo maana falsafa ya sasa ni mchanganyiko wa uzalishaji wa umeme wa aina mbalimbali. Sasa ume-derive hoja nzito sana hapa kwamba Serikali haijaliangalia hili jambo economically badala ya kuwekeza katika miradi ya kuzalisha umeme wa gesi, inawekeza kwenye umeme wa maji…

SPIKA: Waheshimiwa Wabunge kelele zipo nyingi tutulie Mheshimiwa Silinde anapelekwa shule, endelea Mheshimiwa Simbachawene. (Makofi)

MHE. GEORGE B. SIMBACHAWENE: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Silinde anajaribu kutushawishi tuione Serikali imekosea, sisi Wabunge wenzie, Watanzania na dunia kwa kuwekeza katika umeme wa maji megawatt 2100 kutoka kwenye maporomoko ya Mto Rufiji na badala yake tuendelee na gesi ambayo hoja ya kwanza kabisa inaisha, hiyo gesi unayosema inaisha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, unasema size ya bomba… MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Spika, taarifa. SPIKA: Hebu tuvumiliaje kidogo…
WABUNGE FULANI: Aaaah! Kaa chini.

SPIKA: Haya Mheshimiwa Ally Saleh. (Kicheko)

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Spika, ni kweli kama anavyosema, kwa heshima unatakiwa ukae kitako.

Mheshimiwa Spika, ni kweli anachosema kwamba gesi inakwisha lakini jua haliishi, utafiti duniani unaonesha the cheapest ya kufanya umeme ni jua ambalo haliishi, lipo siku zote. (Makofi)

SPIKA: Kuna mawingu siku nyingine, jua halifiki.

MHE. ALLY SALEH ALLY: Una store, sayansi ipo ya kutosha ya kuonesha utafiti wa jua au umeme wa jua unakutosha na una storage, ahsante. (Makofi)

SPIKA: Hayo mabetri ya ku-store umeme usafirishe nchi nzima labda jumba hili dogo. Hoja yake kwamba kuna limitations kwa hiyo energy mixing ni muhimu, nafikiri katika kujenga hoja yake yupo sahihi tu. Endelea Mheshimiwa Simbachawene. (Makofi)

MHE. GEORGE B. SIMBACHAWENE: Mheshimiwa Spika, ninamshukuru Ally Saleh rafiki yangu kwa kusema anatukumbusha pia kwamba tuweke na umeme wa jua, nimezungumza energy mixing means all sources of energy; inaweza ikawa ya makaa ya mawe, vyovyote vile ambavyo vinatoa energy lakini lazima tuwe na mchanganyiko kwa sababu hakuna ambacho ni sustainable, hata hilo jua yako maeneo hayana jua ambayo huwezi ukazalisha umeme. Na ili uhitaji umeme wa jua unahitaji kilometa za mraba nyingi mno kuzalisha megawatt moja, sasa tukienda huko na ardhi yetu na tunahitaji kulima na shughuli zingine za ufugaji, mzee tutapotea hata huko siyo kwa kwenda sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, amenitoa kwenye mstari lakini nirudi. Unazungumzia ukubwa wa bomba la gesi. Essence ya ukubwa wa bomba la gesi kwanza ilikuwa ni ndoto za baadaye, tungeweza kujenga la kipenyo cha sentimita 18, tukaamua kujenga cha 36 kwa sababu tulijua ugunduzi unaendelea na bomba hilohilo litatumika na eneo potential katika uzalishaji/ugunduzi wa gesi ni huko huko kusini. Kwa hiyo, tulipojenga bomba siyo kwamba tuli-equate gesi tuliyonayo leo na tunachokisafirisha, hapana hiyo sio thinking. Kwa hiyo, equation na yenyewe kidogo ina walakini.

Mheshimiwa Spika, lingine ninalopongeza, na nipongeza Kambi ya Upinzani, this time kwenye hotuba yao wameeleza conspicuously kwenye Ibara yao ya 52, msimamo wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kuhusu Mradi wa Rufiji (Rufiji Hydropower Project). Wanasema pamoja na kukubaliana na dhana ya kuzalisha umeme wa megawati 2,100, wamekubali, kwa hiyo hawa ni wenzetu, hawa ni wazalendo ila wana mambo ambayo wanataka tuyatazame. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nadhani Serikali huu ni mchango mzuri wa Kambi ya Upinzani kwamba somo tulilolipiga kwa muda mrefu sasa wamelielewa na tuko pamoja katika jambo hili na ni hotuba hii wamesema hivi, haya maneno mengine tuendee tu kuwaelewesha.

Mheshimiwa Spika, cost of production katika uzalishaji wetu sisi Tanzania iko juu. Tunaposema uchumi wa viwanda hatuwezi kufika huko kama hatuja-deal na hili suala basic la umeme. Na ndiyo maana katika mpango mkakati wa uzalishaji wa umeme nchini tunasema by 2025 tuwe tuna megawati 10,000, megawati 10,000 unazitoa wapi kama una maporomoko kama yale ya Rufiji halafu unayaacha?

Mheshimiwa Spika, hizi kelele za pressure groups duniani zipo tu, huwa zipo tu, tusibadilishe mwelekeo kwa sababu ya kelele za pressure groups, hizi huwa zipo tu. Lakini kuna nchi gani imejitokeza na kusema inaupinga huu mradi, nchi kama nchi; hakuna nchi, ni pressure groups. Kwa hiyo, nasema mmeelewa, ni jambo zuri na sasa tuko pamoja tunakuunga Serikali Waziri kanyaga mafuta twende mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, rai yangu sasa, TPDC mmewawekea mzigo ule wa gharama za ujenzi wa bomba. Ukishaweka gharama za ujenzi wa bomba hatutayaona manufaa ya mnyororo wa thamani wa gesi kwa sababu lile bomba linachukua sehemu kubwa sana ya bei na ndiyo maana negotiation hata ya uzalishaji wa mbolea, negotiation ya kupeleka umeme viwandani bado zinasumbua.

Mheshimiwa Spika, na sisi kwenye Kamati taarifa hizi tunazo. Majadiliano yanasumbua, yako hapohapo kwa sababu wanabiashania visenti, visenti, mwenye kisima aliyegundua gesi – kwa sababu Waheshimiwa Wabunge, gesi haiwezi kuchimbwa na Serikali kwa sababu ile biashara ni risk. Unaweza ukatumia hela za Watanzania wote ambao leo hii tunataka kujenga vituo vya afya, tuna tatizo la elimu, tuna tatizo la huduma za jamii kwa ujumla, ukaenda ukachimba uka-hit dry well na umetumia billions of money. Kwa hiyo kazi hii inafanywa na Private Sector lakini ikishagundua ndiyo mnakuwa na mkataba wa makubaliano ya uendeshaji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa hii ndiyo trend ya dunia nzima. Kwa hiyo, negotiations hizo tukishaweka na bomba la gesi – majadiliano hayaendi ndiyo maana viwanda vya mbolea vimesimama, hakuna kinachoendelea. Tuondoe bomba la gesi tulibebe kama Taifa kwa sababu tunafanya mambo mengi yenye gharama kubwa kuliko hata bomba la gesi, mbona haijawa-pegged? Ina maana standard gauge leo na yenyewe tuiwe TRC, ina maana barabara hizi tuweke TANROADS; itakuaje, tutaendeshaje?

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, uchumi kwa sababu umeme ndiyo utakao-tickle uchumi mzima kuamka ninasihi Serikali ione umuhimu wa kuchukua hii gharama tuibebe kwa ujumla wake. Kwa sababu umeme huu ndiyo unaobeba uchumi pia, tukiongeza hizi megawati maana yake umeme ukisambaa kila mahali uzalishaji unakuwa na bei rahisi, uzalishaji wa bidhaa zetu zitashindana hata kwenye masoko mengine huko duniani. Kwa sasa wanachotushinda wenzetu walioendelea na wanaotuuzia bidhaa ni costal production ambayo number one ni power, sisi umeme wetu ni aghali.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niliomba nitoe rai hii na nikushukuru sana kwa nafasi uliyonipa, na ninaunga mkono hoja. (Makofi)