Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa hii nichangie makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2019/2020. Jana wakati wajumbe wanachangia ilinifanya nikumbuke miaka mitano iliyopita tukiwa ndani ya Bunge lako Tukufu, wajumbe wengi waliokuwa wanachangia baadhi walikuwepo kwenye Bunge lililopita ambalo ilikuwa ikifika kwenye hotuba ya Wizara ya Nishati, wakati huo ilikuwa inaunganika na madini, jambo moja lilikuwa ndio wimbo wa Taifa, lilikuwa gesi; kila mtu alikuwa gesi, gesi.

Mheshimiwa Spika, wakati huo Waziri wa wakati huo Mheshimiwa Muhongo, Profesa, alikuwa akisimama hapo mbele anakwambia sasa Tanzania inaenda kuwa kama Dubai. Sisi wajumbe wa Kamati ya Nishati wakati huo tulikuwa tunasafirishwa kwenda kujifunza gesi. Kila mwisho wa mwezi Waziri anasimama anasema leo gesi imegunduliwa trilioni kadhaa, sasa Tanzania ina gesi zaidi ya trilioni kadhaa, mbili imegunduliwa, tatu, mpaka ikafika hamsini na saba. Tangu ameondoka Mheshimiwa Prof. Muhongo hatujasikia tena taarifa ya ugunduzi wa gesi nchini ambazo zilikuwa zinatangazwa mara kwa mara. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pili, ile gesi ambayo tulikuwa tunaambiwa Tanzania inabadilika kuwa kama Dubai leo hakuna hata mmoja anayeizungumzia tena, tumesahau leo. Sasa leo, jana wajumbe wamechangia nitarudia tena, wakati ule wa gesi imepamba moto Serikali ikaleta mpango kwamba, sasa tunatengeneza bomba refu ambalo lili-cost karibu US Dollar 1.2 billion mpaka Ubungo. Gesi hii italeta umeme wa kutosha, leo bomba lilelile tuliloliimbia wimbo ndani ya Bunge, yaani kila mmoja alikuwa anaimba wimbo, bomba lile linatumika kwa asilimia 6. Six percent mtu ana- justify kwamba, hiyo ndio iko sawasawa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa haya ndio mambo ambayo leo mimi nataka tuyajadili na Serikali itupe majibu. Serikali hapa imeomba kwenye hotuba yake, inaomba trilioni 1.86 ile ya bajeti ya ndani ambayo itakwenda kwenye maendeleo, sawa na 95.1%. Kati ya hizo trilioni 1.44 zinaombwa kwa ajili ya Stiegler’s Gorge, megawati 2,115 ukisoma chini wanakwambia wanaomba bilioni 60 kwa ajili ya extension ya megawati 185. Sasa nataka to think beyond the box na niko tayari kukosolewa; Kinyerezi Extension megawati 185 bilioni 60, hesabu ya kawaida in a layman language ukiwa na bilioni 600 ukafanya extension ya Kinyerezi maana yake una uwezo wa kuzalisha megawati 1,850. Hesabu ya kawaida, ukiwa na trilioni 1.2 una uwezo wa kufanya extension ukapata megawatt 18,000. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa kutumia hela iliyotengwa, kwa mfano ukinipa hela ile ya Rufiji trilioni 1.44 mwakani Tanzania kwa kufanya extension tu itakuwa na megawatt 18,500. Hii trilioni 1.44 ni kwa ajili ya megawatt 2100 ambazo ili zije zikamilike unahitaji trilioni 6. Kwa trilioni 6 unapata megawatt 2115, kwa kufanya extension ya Kinyerezi kwa trilioni 6 unapata megawatt 18,500. Hivi ukijiuliza Tanzania tumerogwa na nani kwenye kufikiri? (Makofi)

MHE. MAULIS S. A. MTULIA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Nani amesimama taarifa?

MHE. SAID M. MTULIA: Mtulia.

T A A R I F A

MHE. MAULID S. A. MTULIA: Mheshimiwa Spika, namheshimu sana mchangiaji na mchango wake ni mzuri lakini nataka nimpe taarifa kwamba kuna tofauti kubwa sana kati ya umeme wa maji na umeme wa gesi.

Mheshimiwa Spika, pesa tunazotumia pamoja na wingi wake kwenye kuzalisha umeme wa maji, yale maji hatutayalipia, hatutalipa bili ya maji, ni maji ya mto. Na umeme utakaotumika wa Kinyerezi I kuzalisha gesi, ile gesi ina gharama tunalipa gesi; kuna pesa kwanza unalipa gesi halafu kuna pesa ya kutengeneza mtambo ambao utatoa umeme. Gesi ni ya TPDC na umeme ni wa TANESCO, lazima ulipe na bei ya gesi, hilo nampa taarifa.

SPIKA: Taarifa hiyo Mheshimiwa David Silinde, unaipokea?

WABUNGE FULANI: Ngoja kwanza, haiwezekani.

SPIKA: Utaratibu hauendi hivyo, tunaenda na mmoja mmoja, aipokee taarifa; hajaongea chochote sasa taarifa yako labda kama unampa taarifa yule aliyeongea kule mwanzo, sasa inakuwa tabu kidogo, Mheshimiwa Silinde.

Waheshimiwa Wabunge, tuokoe muda, leo muda dakika zenu chache sana hapa

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Spika, taarifa ile aliyotoa ndugu yangu Mheshimiwa Mtulia ni suala la kutokusoma na hili ndilo tatizo kubwa sana la nchi yetu, watu hawasomi na poverty mentality imekaa Tanzania, watu hawafikiri. Gesi yenyewe ni mali yetu, siyo mali ya mtu mwingine, ukitumia gesi ukazalisha megawatt 18,500 tutauza Burundi, Rwanda, Kenya na nchi zote kwa kutumia fedha hizi hizi, hela hii inayopatikana tuna uwezo sasa wa kurudi tukaanzisha Stiegler’s Gorge. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa una-ignore jambo moja, unakwenda jambo lingine; unajiuliza tumerogwa wapi? Ndiyo hizi hoja mtu anakuja bwana mnapinga kila kitu kwa sababu ya uchaguzi, kushinda uchaguzi siyo hoja ambayo inatuleta hapa, ni kuishauri Serikali ili iweze kufikia yale malengo. (Makofi)

MHE. CHARLES M. KITWANGA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ambacho nilikuwa nataka kukizungumzia, hoja ya kusema…

SPIKA: Mheshimiwa Silinde naomba, Mheshimiwa nakuruhusu.

T A A R I F A

MHE. CHARLES M. KITWANGA: Mheshimiwa Spika, namuheshimu sana Mheshimiwa anayezungumza ni mdogo wangu lakini asifanye direct costing kwamba ukiwa umetengeneza umeme kwa mwanzo wa shilingi 10 kwa eneo hilo hilo ukifanya kitu kilekile unazidisha mara mbili inakuwa 20. Kuna exponential, kuna extra cost zinazokuwa pembeni ambazo yeye hana details. (Makofi)

SPIKA: Unapokea taarifa ya Mheshimiwa Charles Kitwanga? Makatibu mlinde muda wa Mheshimiwa.

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Spika, nashukuru Wabunge wamenielewa na hata Mheshimiwa Kitwanga amenielewa. Pamoja na kwamba nakubaliana na hoja yake kwa maana ya kunakuwa na other overhead cost it’s true lakini pamoja na hivyo, sikilizeni muwe mnakubali kusikiliza kwanza msiwe mna haraka, sikilizeni muelewe. Hapa tunachoshindana ni ku-think beyond the box, nimefikiria nje na mnavyofikiria ninyi. Kwa hela yenu tutapata umeme mdogo tofauti na hiki ambacho tayari tulishakuwa tumekianza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hapa mmekuja na mpango mzuri tu, kwa mfano issue ya LNG. LNG baada ya ugunduzi wa gesi mwaka 2010, mwaka 2014 Serikali ikasema sasa lazima tuunde LNG ili tuanze kusafirisha gesi. Makampuni yakajitokeza; British Gas, State Oil, Exxonmobil Tanzania, Ofil Energy wakasema sisi kwa umoja wetu tunaweza tukafanya.

Mheshimiwa Spika, mwaka 2016 mwezi Agosti, Mheshimiwa Rais Magufuli akawaagiza TPDC kuharakisha mchakato kwa kuhakikisha LNG inaanza kujengwa, unakuja unasoma ripoti ya Mheshimiwa Waziri anakwambia ndiyo kwanza government negotiation team inakwenda kuanza mazungumzo. Miaka mitano tangu wazo la kuanzishwa kwa LNG, we are still discussing with this mindset Haki ya Mungu hatuwezi kwenda popote, with this mindset hatuwezi kwenda popote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, unajiuliza, nini kinakwamisha? Mwaka 2017 tulitunga sheria nzuri za kulinda rasilimali zetu lakini kuna baadhi ya vifungu havitekelezeki, huo ndiyo ukweli. Juzi juzi nilikusikia ulitoa mfano mzuri tu na nakumbuka juzi wakati Mheshimiwa Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje, Mheshimiwa Mahiga wakati anajibu swali moja akasema mnapoangalia hii mikataba, msiangalie tu upande wa negative, wakati mwingine muangalie mazuri ya mikataba… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)