Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ili nami niweze kuchangia Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati. Niungane na Wabunge wenzangu waliotangulia kupongeza viongozi wetu Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Watendaji wa Wizara hii kwa kazi nzuri na kubwa wanayoifanya; tumepiga hatua kubwa. Ukijaribu kuangalia kulingana na taarifa coverage mpaka sasa hivi vijijini ni karibu asilimia 84 kwa maana ya kwamba kati ya vijiji 12,268 ni vijiji takribani 1990 tu ambavyo havijafikiwa na umeme na ambavyo nina uhakika kwamba 2020 basi tutakuwa tumefika maeneo yote hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika nikienda kwenye mradi wa REA hususan REA awamu ya tatu zipo changamoto ambazo tunaziona hususani katika speed kwa wakandarasi ambao wamepata zabuni hizi. Niombe katika Wilaya yangu ya Ngara usimamizi wa karibu kwa mkandarasi uweze kufanyika.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kama tulivyokuwa tumeanza kwamba tupeleke umeme kwenye maeneo kutokana na uhitaji ambapo kuna huduma za kijamii kama shule, afya n.k. Niombe kwamba katika Jimbo langu la Ngara kama ambavyo Mheshimiwa Waziri ulipokuja; umeshakuja zaidi ya mara tatu; nimekuwa nikikulilia kwamba vile vijiji ambavyo vina huduma hizi, kama Kata ya Bukiriro kwa maana ya kijiji cha Bukiriro, Kijiji cha Mururama kwenda Kigarama, Mrusagamba Tanga, Kumbuga; kwa sababu ya umuhimu na huduma zilizoko kule tunahitaji kupata umeme.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini vipo vijiji ambavyo vilipitiwa na umeme REA II lakini hakuna umeme unaopatikana; kwa mfano Kijiji cha Kenda ambapo line ya kutoka Ngara Mjini kwenda Lusumo boda ilipita pale na ukafanyika uharibifu; kwa maana ya kwamba kuna mazao yaliyokatwa lakini watu hawa hawajaunganishiwa umeme; sawa na Kijiji cha Kata ya Mabawe, Kijiji cha Murugina ambapo pia ulipita line kubwa lakini mazao kama kahawa yalikatwa na bado mpaka sasa hivi wananchi hawa hawajaunganishiwa umeme basi tuweze kuwafikiria hao.

Mheshimiwa Naibu Spika, niipongeze Serikali kwamba tuliunganishwa kwenye grid ya taifa mwaka wa jana lakini mpaka sasa hivi takribani mwaka mzima huduma ya umeme imekuwa ni shida kutokana na msongo wa umeme unaokuja kuwa mdogo, ambao mara kadhaa umekuwa ukikatikana hata kushindwa kukidhi kutoa huduma. Hii imeathiri hata huduma ya maji kwa sababu pampu zinazotumia umeme kusukuma maji zimekuwa haziwezi kufanya kazi vizuri na hivyo kusababisha adha ya ukosefu wa maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunao mradi wa njia ya kusafirisha umeme mradi wa kutoka Rusumo kuelekea Nyakanazi. Line hii ni line ambayo imepelekea kwamba sasa wananchi wanaopitiwa na mradi huo hawajapata fidia mpaka sasa hivi. Mwaka jana kulikuwa na commitment ya Serikali kwamba kufikia mwezi wa tano mwaka jana wangekuwa wamepata fidia lakini mpaka sasa hivi wananchi hawa wa Kijiji cha Kafua, wananchi wa maeneo ya Benako kwenda mpaka Rusumo hawajapata fidia.

Mheshimiwa Naibu Spika, upo mradi tunaoendelea nao katika Jimbo la Ngara ambao ni mradi wa nchi tatu, mradi wa maji wa Rusumo. Mradi huu umekuwa na changamoto kubwa kwa sababu wapo wananchi ambao mpaka sasa hivi ni mwaka wa tatu mradi umeanza hawajapata fidia. Kila ambapo wamekuwa wakijaribu kudai haki hiyo kumekuwa na uzungushwaji hususani Kampuni ya NELSAP ambao wanahusika moja kwa moja katika kuhakikisha kwamba watu hawa wanapata fidia.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Waziri katika hili ajaribu kufatilia kwa karibu ili wananchi ambao wanadai fidia katika mradi huu waweze kupata stahiki yao. Ipo athari kubwa ya milipuko katika eneo hili la mradi ukizingatia kwamba wanapochoronga kwa ajili ya kutengeneza tanel kumekuwepo na mtikisiko mkubwa. Awali ilikuwa ifanyike light blastaling lakini sasa hivi ilipofikia takriban mita 380 ambazo zinatakiwa zichorongwe kwa heavy blasting kuna athari kubwa ambayo itajitokeza na athari ambayo haikuonekana wakati wa kuandaa visibility study na detail design.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba katika vikao ambavyo Mheshimiwa Waziri unahudhuria, vikao vya mawaziri wenye dhamana muweze kuangalia ni namna gani ya kuhakikisha kwamba watu wanapata fidia lakini pia kuangalia namna…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)