Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa fursa. Kwanza nitumie fursa hii kuishukuru Serikali kwa dhati kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Nzega, kile kimeo cha pale Iguguta kimekwisha Naibu Waziri juzi alienda akazindua, Kashishi wameshatuzindulia, nina maombi machache kwa niaba ya wananchi wa Nzega. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba Mkandarasi anayefanya Mradi wa REA wa Nzega asimamiwe. Mradi tuliowasha katika Kijiji cha Ibushi tukiwa pamoja na Mheshimiwa Waziri, mpaka leo nyumba alizoishia ndiyo hizo hizo, wameshindwa kusogeza nguzo wala kupeleka waya. Kata ya Mbogwe mpaka leo umeme haujafika, Sekondari ya wasichana ya Mwanzoli mpaka leo umeme haujafika tumeshindwa ku-enroll watoto wa kike katika hiyo boarding school kwa sababu ya suala la umeme. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Zahanati ya Idudumo mpaka leo umeme haujafika, wametoa commitment by the end of July ikishindikana by the end July Mkandarasi huyu kufanya kazi na Waziri amekuwa very fair kwake kwa sababu ya jinsia, tunaomba wachukue hatua kama Serikali kuhakikisha kwamba suala hili linatatuliwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili ambalo nataka niseme, fairly kabisa mimi nawapongeza TANESCO na Serikali, suala la umeme ration na mgao wa umeme umepungua sana katika nchi sasa hivi, wamefanya hatua nzuri sana na ningetumia fursa hii kusema maneno machache.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama taifa tuna plan ya energy mix, na ukitazama focus ya vyanzo vya umeme ambavyo tunatarajia kupata kutokana na maji vyote tukifanya vitatupatia kama megawati 4,000; ukichukua na megawati 1600 tuliyonayo leo jumla tutakuwa tuna megawati 5600, our target ni kuwa na megawati 10,000 by 2025. Ni muhimu kama Serikali kuanza kujadili sasa hivi ni namna gani vyanzo vya solar vinaanza kutumika, na kama inawezekana tufanye PPP ili watu wa private sector waje wawekeze. Namna gani themo tunaanza kutumia, namna gani mradi wa Singida na Mradi wa Makambako unafufuka, namna gani Mradi wa Mchuchuma unaanza kutekelezwa ili by 2025 tuwe na hizo 10,000 megawati.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo nataka niseme ni kuhusu Stieglers; kumekuwa na national debate kuhusu stiegler’s; hapa tulipofika ni point of no return stieglers must be implemented. Sasa ushauri wangu kwa Serikali tuna mpango wa kuzalisha 2100 megawati kwenye mradi wa Stiegler’s. Swali la kujiuliza do we have a muster plan ya namna gani tutakapoanza kuzalisha 2100 tuta- maintain kwa kipindi cha miaka 10-15 production 2100?

Mheshimiwa Naibu Spika, kama hatutakuwa na grand plan hiyo maana yake investment yote tunayowekeza pale itakuwa ni waste, ni lazima tuangalie namna gani vyanzo vya maji vinavyoenda kwenye Mto Ruaha na Mto Kilombero vinavyopeleka maji kwenye eneo la Stiegler’s vinakuwa protected na namna gani shughuli za binadamu zilizoko katika upper stream zinakuwa marginalized ili vyanzo hivi vya maji viweze kwenda kule. Tusije kujikuta ata the end of the day baada ya miaka 5 stieglers ina-produce 40 percent ya capacity. Baada ya miaka 10 stieglers ina-produce just 50 percent ya capacity. Tuna experience ya Kihansi, tuna experience ya nyumba ya Mungu, tuna experience ya haya mabwawa ya maji. Ni muhimu sana sasa Wizara ya Mazingira, Wizara ya Ardhi, Wizara ya Kilimo kuwa na joint effort ya kutengeneza a grand plan ya ku-protect mazingira katika maeneo haya. Suala la Stiegler’s is national decision ni maamuzi ya nchi we have to do it na kama tunafanya we do it rightly ili ku-attain efficiency and effectiveness.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru naunga mkono hoja (Makofi)