Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Spika, nipende kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nishauri Serikali kushughulikia miradi ambayo ikitekelezwa inachangia pato kubwa kwa Taifa na kwa uchumi wa mtu mmoja mmoja.

Mheshimiwa Spika, napenda kuishauri Serikali kujizatiti kwenye Mchuchuma na Liganga mahali ambapo tungekuza uchumi wa nchi wa urahisi kuliko miradi ambayo yenyewe inakuwa mlaji na si mtoa faida ya haraka na haitengenezi ajira kwa wananchi wengi kwa wakati mmoja.

Mheshimiwa Spika, wananchi wa Ludewa, mahali ambapo kuna Liganga na Mchuchuma wamechoka kusikia maelezo hayo hayo huku uwekezaji ukiwa sifuri. Waziri anapokuja kuhitimisha aje atueleze Serikali imekwama wapi kwenye Mradi wa Liganga na Mchuchuma.

Mheshimiwa Spika, ningependa kuishauri Serikali kufuatilia migodi inayofungwa na kuacha mashimo makubwa yakiwa wazi na yamekuwa hatari kwa jamii yanapojaa maji. Nishauri Serikali kuhakikisha kuwa kabla migodi haijafungwa wanatakiwa kuhakikisha Mikataba yao inasomeka kutokufunga mpaka mashimo yote yamefunikwa.

Mheshimiwa Spika, ningependa kushauri Serikali kuhakikisha inapiga marufuku Wawekezaji wakubwa kuwakandamiza wachimbaji wadogo pale wanapogundua mahali kuna madini.

Mheshimiwa Spika, niishauri Serikali kuhakikisha wachimbaji wanakuwa na bima za maisha kwani wengi wamekuwa wakipata madhila kwa wachimbaji ambapo huishia kufa na kuacha familia ikiwa haina walezi.

Mheshimiwa Spika, nishauri Wizara kuangalia jinsi uchimbaji wa mchanga pia unaacha mashimo makubwa na kuharibu mazingira.